Tuesday, December 30, 2008

CHILDREN TO CHIDREN CLUB.

Na.Mwantumu Jongo.
This is a health club which established for the aims of educating the student about health in the primary level. C to C it is a combinations of students and health’s teachers with the aims to educate about health’s in their schools.

In the early in Shinyanga region there is a problem of the student did not know five basic s of health and it’s a main source of environment pollution.Maarifa resource in cooperation with Radio Sibuka and SNV discover this problem it’s a main source and a take a time and discuss we realise that a children used a many time at school so when educated about health issue through CtoC club because we believe a children had a power to educate the society it is easy to them to protect his /her health and when this children retuned home he or she can at as a good advisers on their families for this perception this C to C club stimulate the development.

A children on C to C club had a capacity to educate society through a songs, comedy, drama and drawing an example when the children see the person goes inverse on the health basics he/she can sing a song with the aim to educate health theme so that person he/she know that’s action it is not good in the society .

Tools&Techniques
Supported Telephone to 8 Primary school at Maswa District which conducted a C to C club.
To express the project at the administration level which include the district commissioner and Regional commissioner?
To build a capacity building to the radio representer, health teachers and student on how to run a c to c club and its duties and obligation .The c to c club was taught 5 basic health on health of environment and personal health, reproduction health, availability of pure water and safety, Immunization against diseases.

RESOUCES
§ Human resources he/she can mobilize the teachers & student to initiated a C to C club in their schools .
§ Fund to manage a Radio Program and facilitator.
§ Telephone and radio inoder a C to C club to listen a live programme and participate fully to share their vies and ideas .


Lesson learned
To have a frequently radio program and money to run this C to C club operation. My suggestion is that insure you have enough money when invest this project at your place and leave the student be free to find out a way to educate the society. Monitoring must be regularly and at a specific time.

Now the student habit changed due to know health basic many school at Tanzania hasn’t a dust bin normally use a hole so it is very difficulty for the newcomer or a guest to keep the environment safety these club hang viroba( plastic bag) at each tree surround school environment when he/she use a solid waste put on the plastic bag in Kiswahili so the school compound was so clean.

Smartness of the student increased due to know personal cleanness her is no wastage of time for a teacher to punish the dirty student because the student educated them selves each an example a student ask other student don’t you know the dirty is not a good habit can cause to you a disease and perhaps the student academic rise d because the student had not get a punishment from the teacher and the student love that teacher .

STRATEGIES
§ To find a radio sponsor inoder the radio Program to be runned at the three months before the contract end to rise awareness.
§ To have a good radio presenter inoder to communicate well with a C to C club to express and share information .
§ To conduct a training on a C to C club to build a capacity for C to C club to be knowledge on how to educate the society.

ADAPT AND APPLY BEST PRACICE
§ First of all introduce the theme or project to the Administration level these include reginal commissioner.
§ Capacity building to the students ,teachers and radio presenter.
§ The student must plan and take ana actions.




AN EXAMPLE OF DUTIES & OBLIGATIONS ON THE HEALTH CLUB

RESPONSIBLE PERSON
DUTIES
TEACHERS
To organise a health club on their school.
To taught a student a how to express their view to the society and how to educate the society through asongs and comedy.
STUDENT
To plan and to do an actions like how to protect their environment through organising public sanitation , how to get ana excess on pure water and implement their plans .
REPRESENTER
To insure that the radio programme sustanablility.

§ Arrange the live Radio Program and the student express their view to the public.
§ Monitoring and revaluation through the study visity the student can move from one school to another to learn what other practice.

MKOJO WA KONDOO HUHIFADHI MBEGU ZA MAHINDI

Na.Mwantumu Jongo.
Mbegu za mahindi huhifadhiwa ili zisiharibiwe na wadudu kwa kumwagiwa mkojo wa kondoo .Kuna njia nyingi za kuhifadhi mazao yetu lakini wasukuma wamenitolea kali ya mwaka kwani wao wanahifadhi mbegu zao za mahindi kwa namna ya pekee tumezoea kuona mbegu hii zikihifadhiwa kwa kufungwa mahindi pamoja na majani yake na kuhifadhiwa juu ya dali la jiko ili ziweze kukaushwa na moshi wa jikoni.

Lakini katika eneo la Kitangili lililopo karibu na stesheni ya reli mjini shinyanga ndipo nilipokutana na uvumbuzi wa aina yake kwani bwana Kulwa Steven alisema tangu utoto wao huhifadhi mbegu za mahindi kwa kutumia njia hii .

Ambapo mkulima hutayarisha “jeka”ni sehemu ya kuhifadhia mbegu kama vile ilivyo mtungi .Kuna njia mbili za kujenga jeka,mahitaji yake ni kamba ,miti mirefu na mifupi na mabua.Katika njia ya kwanza mkulima hutafuta miti mirefu , na nguzo fupi anachimbia chini ya ardhi ,kisha analaza fito mstari mmoja halafu zile mbegu za mahindi anazifunga kwa kuyaunganisha majani ya yale mahindi yenyewe kwa yenyewe na kuanza kuyapanga kwenye fito njia hii kwa kisukuma huitwa nshijite .

Njia ya pili ni ile Mkulima hutafuta miti mirefu na mifupi anatengeneza kichanja halafu pembeni anasimamisha miti mirefu halafu anasiliba na mabua unaweza ukatengeneza kajumba kwa juu ili kuzikinga mbegu zako katika kipindi cha kiangazi .

Mkulima huchukua mahindi mabichi hayatoi majani yake unayaunganisha na kuyafunga pamoja kisha unayahifadhi kwenye jeka lake .Vijana hutumwa kuleta mkojo wa kondoo ambao hupatikana kwa kumshika kondoo na mwengine hukinga ule mkojo inasemekana kondoo ni nadra kukojoa lakini akishikwa hukojoa haraka na kumwagia katika jeka lenye mbegu za mahindi .Mbegu za mahindi huweza kuhifadhiwa kwa njia hii kwa muda wa mwaka mmoja na zaidi bila kuharibiwa na wadudu.

Bwana Steven anaamini wadudu hawapendi harufu ya mikojo ya kondoo hivyo wakikaribia katika jeka huondoka mara moja na kuziweka mbegu zao katika hali ya usalama .
Kwa upande wangu nimebahatika kuona njia nyingi za kuhifadhi mbegu za mahindi kama vile kuhifadhi katika mti wenye njia panda unalaza mti na kuyafunga mahindi yako nji hii na nyinginezo hutumika sana katika vijiji vingi nchini Tanzania hivyo hatuna budi kuzitumia ili tuweze kuwa na uhakika wa kuhifadhi mbegu za mahindi.
Serikali na taasisi binafsi ziziendeleze njia hizi za asili kwa kufanyia utafiti ili kuwa na uhakika zaidi wa ubora wa njia hizi kwani tukumbuke kuna usemi usemao kuwa ya kale ni dhahabu.

KILIMO MSETO NA MAENDELEO YA JAMII

Na.Mwantumu Jongo.
Kilimo mseto ni elimu iliyomuwezesha Ndugu Joseph Seni na wakulima wengine kupata maendeleo ya haraka .Katika nchi yetu kilimo mseto ni moja ya kilimo kilichokuwa kikifanywa na babu zetu ingawaje hawakutambua kama walikuwa wakifanya kilimo hiki wazee wa zamani walikuwa wakiachia aina fulani ya miti mashambani ili kupata kivuli kama sehemu ya kupunzikia shambani ,wakiachia miti ya matunda na miti mingine ya dawa mashambani ,miti iliyokuwa ikiachwa ni miti ambayo ilikuwa haidhuru mazao na inapukutisha majani yenye kuongeza rutuba ardhini ,pia walikuwa wakihifadhi eneo Fulani la malisho kwa ajili ya ndama na ng’ombe wagonjwa hii yote ilikuwa ni namna ya kilimo mseto.
Baada ya uharibifu mkubwa wa mazingira kuanza kutokea wataalamu waliamua kuboresha kilimo asilia na kupata kilimo kijulikanacho kama kilimo mseto elimu ambayo kwa sasa inahitajika sana ili kunusuru hali ya uharibifu wa mazingira duniani.
Mchungaji Joseph Seni ni mkazi wa kijiji cha Mwasele Lubaga tangu mwaka 1994 alianza na shamba la kilimo lenye ekari mbili na kutokana na mafanikio ameweza kununua shamba jingine hadi kufikia hekari nne(4).Bwana mstaafu wa kanisa la (PEFA)pentecoste Evangelistic Fellowship Africa Shinyanga ,alistaafu kazi ya uchungaji na kujiunga kitengo cha uinjilisti uenezi mwaka 1994 na baada ya kustaafu uchungaji bwana Joseph Seni aliweza kuanzisha kilimo mseto kwa kutekeleza baadhi ya vifungu vya Biblia vinavyohusu utunzaji wa mazingira .
Mchungaji huyo ni miongoni mwa wakulima waliopata mafanikio makubwa baada ya kupata elimu ya kilimo mseto baada ya kuona mafanikio yake mchungaji amejitolea kuelimisha jamii kuhusu kilimo hiki na manufaa yake kwa kuanzisha vikundi vya kilimo mseto na ngitili ,utayarishaji na uhifadhi wa malisho kwa njia bora.Biblia kwa kutumia maandiko matakatifukutoka katika kitabu cha mwanzo 2:8na mwanzo 2:15 mchungajiamefanikiwa kushawishi watu wengi kuanzisha shughuli za utunzaji wa mazingira .

Mwanzo 2:8 inaeleza yafuatayo ;
‘Bwana mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni akamweka ndani yake mwanandamu .
Mmwanzo 2:15
Bwana mungu akamtwaa huyo mtu akamweka katika bustani ya Edeni ailime na kuitunza’kwa kutumia maandiko matakatifu yaliyotajwa ni kwamba yanaikumbusha jamii ya kuwa dunia iliumbwa na kuwekewa mazingira mazuri ila kwa matumizi ya mwanandamu ndiye aliyeanza kuyaharibu mazingira yake hivyo inatupasa tuyatunze kama mungu alivyotuamuru ni dhahiri kwamba bwana aliweza kueleweka vizuri .
Siri ya mafanikio ya mchungaji ni kwamba pamoja ya kusoma maandiko matakatifu ndani ya biblia aliweza pia kujisomea kitabu chake kiitwacho ‘Mkulima stadi(P.Otma Monger OSB na P.B Ngeze NdandaPublication 1941,1985)ambacho kinaelezea fani mbalimbali za kilimo na ufugaji aliwahi kukutana na mkulima mmoja bwanan Antony Katakwa ambaye tayari ameshaanza kilimo mseto kwa msaada wa Shinyanga Mazingira Fund.
MAFANIKIO
Ndugu Joseph amefanikiwa kusambaza elimu hii kwa watu wengi ikiwa ni pamoja na kikundi cha Juhudi na maarifa group na makundi ya kikristo mfano mzuri Mwamagunguli,Iselamagazi PAG ,Mongolo Kahama PEFA,Muhina Mwamapalala Maswa .
Kuanzisha bustani za miti Iselamagazi,mwamagunguli,Kitangiri na Chibe.
Alianza na ufugaji wa kuku wakaongezeka hatimaye kubadilishana kupata mbuzi na hatimaye kupata n’gombe .Ameweza kuongeza shamba kutoka ekari 2 hadi 4 kwa sasa .Ameongeza mavuno katika shamba lake kutoka gunia moja(1) hadi kumi na sita(16)za mahindi kwa ekari tatu .
Ameweza kuanzisha shamba la malisho yanayotosheleza mifugo yake na ziada anauza na kupata kipato .
Ameweza kuanzisha ufugaji nyuki .Ameboresha maisha yake na kutengeneza nyumba bora ya bati.
MATARAJIO YAKE
Anatarajia kubadilisha mifugo ili apate ng’ombe wa maziwa ,kuanzisha bustani ya matunda ,kuanzisha bustani ya kuzalisha uyoga.
Pia anatarajia kutoa elimu kwa vijanailia wapate kujiajiri kupitia rasilimali zinazopatikana kwa kutunza mazingira.
USHAURI
Kutokana na tafiti mbalimbali za kilimo mseto zimeonyesha kuwa jamii inaweza kufaidika sana kwa kulima kilimo hiki kwani kilimo mseto kimeshafanyiwa utafiti kwenye makundi makuu manne ambayo yanamsaidia mkulima ,mfugaji mifugo,mfugaji wa nyuki na mfugaji wa samaki kwenye eneo dogo kupata kipato kiubwa .
Ni vizuri tuige mfano wa mchungaji Josepaliyeweza kutumia eneo dogo la kilimo na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kutoka katika eneo moja.

UVUNAJI WA MAJI KWA NJIA YA MAJALUBA

Na.Mwantumu Jongo.
Kitangili ni eneo linalopatikana katika wilaya ya Shinyanga mjini baadhi ya wakazi wake wanalima mpunga kwa kutumia mitaro badala ya maji ya mvua kumwagika ovyo yanaelekewa kwenye mashamba maarufu kama majaluba.Majaluba ni sehemu iliyoandaliwa kwa ajili ya kupanda mpunga.Njia hii husaidia sana katika kuhifadhi maji hususani katika maeneo ya nyanda kame ili kuweza kuongeza uzalishaji katika eneo dogo.

Upatikanaji wa maji katika majaruba unafanyika kwa kutengeneza mitaro inayotiririsha maji na kuielekeza kwenye majaruba. Utengenezaji mitaro unahitaji ushirikiano hasa pale kunapokuwa na majaruba mengi yanayomilikiwa na wakulima mbalimbali.

Hivyo mitaro hii hutengenezwa na wakulima kwa kuyaelekeza maji ya mvua katika majaruba yao. Njia hii imekuwa na manufaa sana kwani hakuna maji yanayoachwa ovyo. Kwa hiyo hii ni namna mojawapo ya utumiaji mzuri wa maji.

Hali hii imewafanya wakulima wengi kupanua mavuno yao. Awali mkulima alingoja mvua tu huku miteremko ya maji ikitiririsha maji ovyo. Baada ya ugunduzi huu wa taaluma hii, wakulima wamejikuta wakinufaika sana. Sasa hivi wakulima wamenzisha vikundi vya kutengeneza mitaro ya namna hii katika azma ya kuboresha kilimo cha mpunga.


UTAYASHAJI WA JARUBA
Unalima na kuweka kingo nne za matuta baada ya siku saba unayachanganya majani yaliooza na udongo ni mbolea. Majani yasiyooza unayalundika pembeni ya shamba ili yasiote huchanganywa na udongo baada ya mavuno hutumika kama mbolea. Unaangalia uelekeo wa maji ardhi iwe sawa ukiona kilima unashushia kwenye bonde hii inasaidia kutunza maji kwani mpunga unahitaji maji mengi.Hakikisha miche ya mpunga haizami kwenye maji .

KUOTESHA MBEGU
Kipindi cha mwezi wa kumi mkulima huotesha mbegu kwa ajili ya kilimo cha mpunga kuna njia mbili za kuotesha mbegu njia ya kwanza ni ile ya kulima kitalu pembeni ya jaluba sehemu yenye unyevu nyevu na kuotesha mbegu zikiota miche ikikuwa ndipo huhamishwa na kupanda kwenye majaluba yaliyoandaliwa .
Aina ya pili ni kutifua jaluba na unamwaga mbegu za mpunga ndani ya jaluba zima kwa kusubiri mvua ili mbegu iote.

UPANDAJI
Miche ikikuwa unangoa na kupanda katika jaluba katika njia ya pili kama imeota miche imeota mingi unahamisha na kupanda katika jaluba jingine eneo likiwa na rutuba nyingi unapanda mche mmoja.Majaluba yan milango ya kupokea maji na kutoa mfano mpunga ukianza kucahnua unahitaji maji hivyo milango yake huwa wazi ili kuingiza maji kwenye jaluba.
UPALILIAJI
Kwenye jaluba kukiwa na maji ya kutosha majani yanakufa kwa kuoza katika maji ardhi inakuwa laini mkulima huyangoa na mkono lakini unatakiwa uchukue tahadhari kwani majani ya mpunga yanafanana na magugu hivyo unashauriwa usubiri hadi miche ifikie inchi kumu na tano(15).
UVUNAJI
Baada ya takriban miezi mitatu, uvunaji wa mpunga huanza. Uvunaji uko katika njia mbili nazo ni (a) uvunaji wa kutumia kisu kwa kukata kila kikonyo cha mpunga (b) uvunaji wa kutumia kiberenge yaani kukata shina lote la mpunga kwa kukusanya katika makundi makundi.
Kisha unaandaa sehemu safi ambayo itakuwa haina mchanga. Eneo hili utatumia jembe kuondoa nyasi na mchanga. Fagia eneo lako kwa kuondoa mchanga. Pale inapobidi, unaweza kutumia mavi mabichi ya ng’ombe kwa kuyafanya yawe mazito kiasi. Changanya katika ndoo hakikisha hakuna mabonge mabonge ya mavi ya ng’ombe.
Chukua mfagio mgumu wa nje na kumwaga huo mkorogo wa mavi ya ng’ombe. Fagia mkrogo huo na kuacha mwingine unate sehemu uliyoandaa. Ukisha kamilisha acha pakauke. Unaweza ukapaacha pakauke kwa muda wa masaa mawili au matatu na kuanza kazi.
Somba mpunga wote uliokata na kuurundika katika eneo uliloandaa kwa ajili ya kupigia. Daima unapoleta panga katika mstari katika duara kwa kurundika ukiacha nafasi kigodo katikati. Anza kuchukua kiasi unachoweza kukiwebeba mikononi na kukiinua juu kisha kipigize sehemu uliyoacha wazi. Pigiza mara tatu au nne kutegemea hakuna mpunga unaosali kwenye majani ya mpunga. Endelea hadi rundo lako limekwisha.

Kama kuna mpunga mwingine, endelea kufanya hivi mpaka umalize. Ukiona umechoka, unaweza kuamua kupeta mpunga uliopiga kwa kutumia ndoo. Chota mpunga kadri unavyoweza kubeba na kuinua juu pembeni kidogo mwa mpunga uliopiga. Mwaga kidogo kidogo utaona pumba na uchafu mwingine unapeperushwa na upepo.na hivyo mpunga safi kubaki karibu na miguu yako. Endelea mpaka umalize rundo la mpunga uliopiga.
Kazi itakayofuata ni kuweka katika mifuko unashona na kusafirisha nyumbani.Kazi ya uvunaji itakuwa imekamilika.
Uvunaji wa kukata kila kikonyo cha mpunga unafanyika kwa uchache sana kwani unapoteza wakati mno na pia nguvu nyingi. Mpunga unapokuwa umevunwa, huwekwa ndani kwa muda wa mwezi mmoja au miezi miwili ili ukauke vilivyo. Hatimaye eneo maalum la kupigia kama nililolieleza hapo juu huandaliwa. Mpunga hutolewa nje na kuachwa kwa muda mfupi ukauke. Kazi inayofuata ni kupiga mpunga kwa kutumia fimbo ndogo ndogo. Upigaji huu ni wa kuhakikisha kuwa hakuna mpunga unasalia kwenye vikonyo vyote.
Kazi ya kupeta inafuata baada ya kumaliza kupiga. Baada ya kupeta mpunga hujazwa katika magunia ama huwekwa katika ghala.

MAFANIKIO
Mavuno mengi katika eneo dogo.
Shamba kuwa na rutuba
Kukiwa na maji ya kutosha kama kukiingiliana na mto kuna uwezekano mkubwa wa kupata samaki.

MATATIZO
Wadudu waitwao ngegeshi hupatikana wakati maji yakiwa yamepungua hukata majani ya mpunga.
Ndege ambao kwa sasa hutumia njia za kienyeji kuwa fukuza kama kuchonga masanamu yanayofananna na watu,kanda za redio hufungwa pembeni mwa kingona hata mabetri hubondwa na lie bati lake kwa vie tu lina mngao huwakimbiza ndege.

SUNGUSUNGU WATUNZA MAZINGIRA

Na.Mwantumu Jongo.
Wengi wetu tumekuwa tukifahamu kuwa sungusungu ni jina la wadudu wadogo wadogo weusi ambao hutambaa ardhini.Wadudu hawa huuma pindi wanapokandamizwa.Mtu aumwapo na wadudu hawa huisi uchungu. Neno hili lilipendekezwa litumike kwa kikundi hicho cha Usalama kwa sababu ya kujihami kwao kwa haraka wawapo na tatizo.
Licha ya kwamba sungusungu hawa adhabu zao haziendani na sheria ya nchi mfano mzuri aliyetengwa haruhusiwi katika kufanya ibada lakini wana mchango mkubwa katika kutunza mazingira yetu.

“Kutunza mazingira ni sehemu ya kazi yao “alisema bwana W.C.Mlenge.
NAFRAC ilipoanza mradi ilikuta sungusungu imeshatawazwa . Mnamo mwaka 1992 mwezi wa saba walienda Bariadi kufanya utafiti wa taasisi za kiasili zitasaidiaje katika kutunza mazingira wakaitisha mkutano wakiongozwa na chifu wao wa zamani ambaye alijua mambo ya mila na uhusiano mzuri (Mhola)Dagashida waliendesha mkutano vizuri.
Ndipo tulipooona dhahiri kuwa wahenga hawakukosea waliposema tunza mazingira nawe ya kutunze ni usemi uliokuweko toka enzi za mababu zetu sungusungu hawa waliweza kutunza mzingira yao kwa vitendo .
Toka jadi wao ndio walikuwa walinzi wa misitu ya asili hawakuishia hapo walikuwa wanalinda kisima kisichafuliwe kwa kutunza misitu ulio karibu na kisima ili kiwe na maji mengi .
sungusungu walianzisha na kuyatunza maeneo mengine ya kulishia mifugo maarufu kama ngitili hao ndio walikuwa walinzi wakuu mfano mzuri katika vijiji vya Ikonda,Busongo,Mwamishani wanataratibu zao za kutunza ngitili kwa kufanya hivyo waliweza kupunguza kulishia mifugo eneo bila ya ruhusa ya mwenye eneo hilo ukikutwa walikuwa wanakuadhibu kisheria .

Pia waliweza kutatua migogoro ya mipaka ya mashamba katika eneo lao hii ilisaidia katika jamii za kisukuma kuishi kwa amani na upendo .Sungusungu wapo katika kamati za mazingira hivyo hutoa mawazo mazuri katika utunzaji wa misitu ya asili na wao ndio watekelezaji wakuu wa suala zima la utunzaji wa mazingira.
Kuwinda ,kuchunga na kukata miti kulikatazwa kulifanywa kwa ruhusa maalum kutoka kwa mwenyekiti wa sungusungu ukikutwa unalipa faini hii ilisaidia sana jamii ya kisukuma kuweza kuwa na mazingira yaliyoboreshwa kiukamilifu.
Nilikuwa na kiu ya kujua asili hasa ya sungusungu ni nini ndipo hapo bwana mwenyekiti wa sungusungu wa Lubaga aliponielezea sungusungu ilianzishwa mwaka 1982 katika kijiji cha ng’wang’halanga wilayani Nzega. Mzee Mwanamabonde alianzishwa sungusungu baada ya kukutwa na watu walokuwa wameibiwa ng’ombe.
Basi Mwanamabonde akiwa mwenyekiti wa kijiji hicho aliwaambia kuwa pamoja na ng’ombe kuwa wako kwa bwana Pandasahani, itakuwa ni vigumu au haitawezekana ng’ombe hao muwachukue hivi hivi tu.

Mzee Mwanamabonde akawaambia tulieni hapa kwanza. Basi Mwanamabonde akaitisha mkutano wa wanakijiji wake kisha wakaenda pamoja nao kwenye mji wa Pandasahani ambapo ng’ombe mbalimbali wa wizi walitunzwa hapo.

Ilikuwa ni siku Pandasahani alikuwa ameamua kufanya karamu kwani walikuta ng’ombe amechinjwa, nyama zikipikwa jikoni. Jamii iliyochoshwa na vitendo vichafu vya Pandasahani iliwaamuru wake zake Pandasahani kujitwisha vyungu vya nyama kutoka jikoni bila kujali wanaungua kiasi gani. Pandasahani aliambiwa wanapelekwa kituo cha Polisi. Wakiwa pamoja na Pandasahani na familia yote, waliongozwa hadi katikati ya pori ambako waliambiwa kuwa hapa ndiyo kituo cha Polisi.

Waliamuriwa kusali mara ya mwisho kwani siku zao zilikuwa zimekwisha. Sahani na familia yake yote kila mtu kwa wakati wake alisali. Utesaji ulipoanza kwa akina mama kwa kukatwa ziwa moja huku wakiwa hai bado. Hatimaye akina baba nao walionja joto ya jiwe kwa kukatwa sehemu za siri wakiwa hai. Kazi ya mwisho ilikuwa kuuwawa kwa familia ya Pandasahani. Maiti zao ziliachwa porini.
Baada ya kubainika mauaji haya, polisi walikuja, lakini mzee Mwanamabonde alikana akasema hajui kwani halikuwa eneo lake. Polisi wakamwacha huru.

Mzee Mwanamabonde akazuru Kahama kueneza mbinu za kuanzisha Sungunsungu. Akiwa wilayani Kahama, alikutana na mzee Kishosha, mzee Jugi na wengine walioonekana wazuri na maarufu. Aliwaelezea azma yake ya kuanzisha sungusungu. Aliwapa mbinu aliyokuwa akitumia huko kwake.

Harakati hizi za kuanzisha sungusungu zilizagaa na kutafsiriwa kuwa wanaanzisha chama cha siasa. Mkuu wa wilaya Kahama alimwarifu Rais kuwa kuna chama cha siasa kimeanzishwa Kahama. Rais aliagiza mara moja watu hao wafunguliwe na mashitaka. Kweli muda mrefu haukupita watu hawa akina mzee Jugi, mzee Kishosha na wengine wakahukumiwa kifungo cha miezi kumi kila mmoja.

Tume iliteuliwa baadaye walifanyia uchunguzi chama hiki. Katika Tume hiyo akiwemo Mbunge wa Maswa Mheshimiwa Shillingi na wengine. Katika kuwahoji wazee hao waliokuwa wakituhumiwa, Mheshimiwa Shillingi aliwataka waongee kisukuma. Wazee hawa kila mmoja alidai wamechoshwa na wezi. Hapakujitokeza suala la kisiasa hata kidogo.

Tume ikawasilisha taarifa yake kwa Mheshimiwa Rais, muda si mrefu Rais akamuru watu hao waachiliwe mara moja na waendelee kuunda sungusungu yao kwa minajili ya ulinzi wa ng’ombe wao na mali zao nyingine. Katika eneo la Lubaga sungusungu wamefanikiwa kwa kiasi kikiubwa katika utendaji wao wa kazi za kila siku na kusaidia watu kuishi katika amani na usalama.chombo bila nahodha huenda mrama ndivyo inavyokuwa sungusungu wa Lubaga wao kama wao wana utawala wao.
Hakika jeshi la jadi halikuwa na mzaha hata kidogo kwani katika utawala wake kulikuwa na Mtemi (Ntemi) ambaye alichaguliwa kwa kigezo cha kuwa na maarifa ya tiba za jadi au za asili ,na huacha madaraka kwa muda wa miaka mitatu labda aumwe,afe,ahame ndio amejivua uongozi na uongozi haufuati ukoo fulani bali huchaguliwa na wananchi wenyewe.msaidizi wake aliyeitwa Mwambilija “Mtwale”,katibu wake aliitwa mwandiki na msaidizi wake pia kuna kamamanda mkuu aliyetwa kwa jina la asili la Nsumba ntale na wajumbe wa kamati.Katika uongozi wao hawana kiongozi mwanamke kwa minajili ya kwamba wanawake hawawezi kutunza siri lakini kwa uchunguzi tulioufanya kuna matawi mengine kuna wenyeviti wanawake mfano mzuri ni katika kijiji cha Mwagala.
Katika jamii ya wasukuma kuna kuwa na penga mbili (filimbi)viongozi wa familia wanakuwa nazo yaani mama na baba popote wakitokewa na tatizo wanapiga sungusungu na watu wengine wanakuja na katibu anaandika tatizo lililotokea .
“Ndulilu”ni kipande cha kibuyu kilichotobolewa katika sehemu tatu na sehemu mbili zinazibwa sehemu moja inatumika kwa kupiga endapo tu kuna tatizo kubwa mfano wizi wa mifugo na mauwaji.
Tukumbuke kuwa ulinzi wa jadi ni sheria ndogondogo tuliojiwekea ili kujilinda na mali zetu .Endapo mtu ameenda kinyume na sheria tuliojiwekea hupewa adhabu maarufu kama kupigwa “mchenya”ambazo ni faini ndogo ndogo na ukiendelea wanakutenga (kumtulija)ina maana usishiriki katika shughuli zote za jamii ukifiwa watu wanakuja kuzika lakini sungusungu wanawafukuza ndugu zako kuwafariji na kulala matangani na ukifa utakuwa umeikomboa jamii yako.Ukiwa mjeuri,mwizi,unaharibu mazingira kwa kiasi kikubwa unapelekwa kujikomboa katika jeshi jingine na unatozwa faini kubwa Na adhabu zao haziangalii jinsi wala umri.
Kila kwenye mafanikio hakukosi kuwa na matatizo ndivyo ilivyo kwa wenzetu hawa sungusungu hawana vifaa vya ulinzi vya kisasa ,isitoshe kuna watu ambao hukutwa nyakati za usiku lakini si wezi na kwa upande wao yaani sungusungu wenyewe wanakuwa wanakiuka miiko yao kwa kuwa wanafiki na wenye majungu hivyo kukwamisha zoezi zima la ulinzi .
Licha ya hayo kuna mafanikio ambayo wameyapata ni kupungua kwa wimbi la wizi wa mifugo kwani vijana ndio hasa wenye ari na wito wa kulinda nchi yao na mali zao.
Sungusungu wanautaratibu wa usambazaji wa taarifa kwenda tawi jingine ujulikanao kama mwano ni taarifa ya hatari kutoka tawi moja kwenda jingine endapo kuna tatizo limetokea ili waweze kusaidiana kulitatua .Endapo mifugo imepatikana katika tawi jirani huwaarifu na kwenda kuchukua ,au wezi wamepatikana n.k.
Ikiwa mali imepatikana Mwenyewe asipopatikana kwa upande wa mifugo inatunzwa na kutangazwa kwenye matawi ya jirani baada ya miezi sita inakuwa ni mali ya sungusungu na fedha inayopatikana kutokana na faini au mifugo iliyookotwa hupelekwa katika ujenzi wa maendeleo kama vile shule na hospitali.
Kwa hali ilivyo sasa hivi kila mti una mwenyewe ukikutwa umekata mti unapelekwa kwa sungusungu na sungusungu wanakuhukumu.
Kwa upande wangu naona sungusungu ni wazuri katika suala zima la utunzaji wa mazingira hivyo basi sisi wananchi inabidi tuwaunge mkono sungusungu na kwa upande wao basi walegeze adhabu kwa aliyetengwa angalau aweze kushiriki katika masuala ya kidini tofauti na ilivyo sasa.

Serikali kutambua fursa hii iliyopo ya ulinzi wa jadi(sungusungu) ikizingatia suala la ulinzi shirikishi ambao umeonyesha mafanikio makubwa kwa taifa hili hususani vyombo vya ulinzi kwani jamii inachukua nafasi kubwa kama chanzo cha habari.
Mafunzo kwa taasisi za namna hii ni muhimu sana ili kuongeza ufanisi zaidi kwa kuzingatia ukweli na uwazi.

EPUKA SUMU;TUMIA JIVU LA MAJANI YA VIAZI HUHIFADHI MAPALAGE

EPUKA SUMU;TUMIA JIVU LA MAJANI YA VIAZI HUHIFADHI MAPALAGE

Hakika sasa jamii za nyanda kame zinatafuta njia hasa ya kuendana na mazingira yao kwa kuweza kugundua njia mbadala za asili kuhifadhi mazao yao ili yasiliwe na wadudu bila kutumia chemikali za viwandani ambazo zimedhihirika kuwa zina madhara makubwa kwa binadamu.Hii inawapa usalama na uhakika wa upatikanaji wa chakula kwa mwaka mzima na pia inawasaidia kuondokana na tatizo la uhaba wa chakula hususani katika kipindi cha kiangazi.

Mapalage ni viazi vitamu ambavyo humenywa na kukatwa katika vipande vidogo vidogo mfumo wa chips. Chakula kinachopendwa sana katika jamii ya wasukuma kwani hutumika sana katika kipindi cha kiangazi

Jamii ya kisukuma nayo haiko nyuma kwani haitaki kupitwa na wakati wameweza kugundua njia mbadala ya uhifadhi wa mapalage ili kuwawezesha kuwa na uhakika wa kupata milo yao ya kila siku.

Jamii hii huweza kuhifadhi mapalage kwa kutumia jivu la majani ya viazi kwa muda mrefu ili yasiweze kuliwa na wadudu. Wamekuwa wakihifadhi mapalage katika njia mbili, njia ya kwanza ni kuvipika viazi bila ya kuvimenya vikisha iva huvikata katika vipande vidogo vidogo yaani matoborwa na njia ya pili ndio hasa iliyonifanya niandike makala hii kwani ni ya aina yake! jamii ya kisukuma hutayarisha viazi kwa kuvimenya na kuvikata katika vipande vidogo vidogo na majani ya viazi huanikwa badala ya kutupwa au kuliwa na mifugo kama tulivyozoea, yakikauka huchomwa moto na majivu yake hutunzwa tayari kwa kuhifadhia mapalage .

Mapalage yakishakauka huhifadhiwa kwenye gunia; Hatua ya kwanza kabisa msukuma huweka jivu la majani ya viazi halafu huweka mapalage yake kwa ajili ya matumizi ya baadae. Faida ipatikanayo kutokana na njia hii ya kuhifadhi mapalage huweza kukaa hata mwaka mzima bila ya kubunguliwa na kuharibiwa na wadudu.
Hivyo huwa na uhakika wa familia zao kupata chakula kwa mwaka mzima kwani wao viazi vitamu ndio zao linalilovumilia ukame na hivyo hustawi vizuri katika ardhi yao.
Msukuma hupika mapalage yake kama vile futari kwa kuyaunga na karanga au mafuta huweza kutumiwa kwa kweli ni mlo kamili.
Kwa mtazamo wangu njia hii ya asili ni nzuri badala ya kutumia madawa ya viwandani yenye kemikali ambazo huleta athari katika miili yetu watu wanaweza kutumia njia hii ili kuweza kuhifadhi viazi vitamu

SUNGUSUNGU WATUNZA MAZINGIRA

Na.Mwantumu Jongo.
Wengi wetu tumekuwa tukifahamu kuwa sungusungu ni jina la wadudu wadogo wadogo weusi ambao hutambaa ardhini.Wadudu hawa huuma pindi wanapokandamizwa.Mtu aumwapo na wadudu hawa huisi uchungu. Neno hili lilipendekezwa litumike kwa kikundi hicho cha Usalama kwa sababu ya kujihami kwao kwa haraka wawapo na tatizo.
Licha ya kwamba sungusungu hawa adhabu zao haziendani na sheria ya nchi mfano mzuri aliyetengwa haruhusiwi katika kufanya ibada lakini wana mchango mkubwa katika kutunza mazingira yetu.

“Kutunza mazingira ni sehemu ya kazi yao “alisema bwana W.C.Mlenge.
NAFRAC ilipoanza mradi ilikuta sungusungu imeshatawazwa . Mnamo mwaka 1992 mwezi wa saba walienda Bariadi kufanya utafiti wa taasisi za kiasili zitasaidiaje katika kutunza mazingira wakaitisha mkutano wakiongozwa na chifu wao wa zamani ambaye alijua mambo ya mila na uhusiano mzuri (Mhola)Dagashida waliendesha mkutano vizuri.
Ndipo tulipooona dhahiri kuwa wahenga hawakukosea waliposema tunza mazingira nawe ya kutunze ni usemi uliokuweko toka enzi za mababu zetu sungusungu hawa waliweza kutunza mzingira yao kwa vitendo .
Toka jadi wao ndio walikuwa walinzi wa misitu ya asili hawakuishia hapo walikuwa wanalinda kisima kisichafuliwe kwa kutunza misitu ulio karibu na kisima ili kiwe na maji mengi .
sungusungu walianzisha na kuyatunza maeneo mengine ya kulishia mifugo maarufu kama ngitili hao ndio walikuwa walinzi wakuu mfano mzuri katika vijiji vya Ikonda,Busongo,Mwamishani wanataratibu zao za kutunza ngitili kwa kufanya hivyo waliweza kupunguza kulishia mifugo eneo bila ya ruhusa ya mwenye eneo hilo ukikutwa walikuwa wanakuadhibu kisheria .

Pia waliweza kutatua migogoro ya mipaka ya mashamba katika eneo lao hii ilisaidia katika jamii za kisukuma kuishi kwa amani na upendo .Sungusungu wapo katika kamati za mazingira hivyo hutoa mawazo mazuri katika utunzaji wa misitu ya asili na wao ndio watekelezaji wakuu wa suala zima la utunzaji wa mazingira.
Kuwinda ,kuchunga na kukata miti kulikatazwa kulifanywa kwa ruhusa maalum kutoka kwa mwenyekiti wa sungusungu ukikutwa unalipa faini hii ilisaidia sana jamii ya kisukuma kuweza kuwa na mazingira yaliyoboreshwa kiukamilifu.
Nilikuwa na kiu ya kujua asili hasa ya sungusungu ni nini ndipo hapo bwana mwenyekiti wa sungusungu wa Lubaga aliponielezea sungusungu ilianzishwa mwaka 1982 katika kijiji cha ng’wang’halanga wilayani Nzega. Mzee Mwanamabonde alianzishwa sungusungu baada ya kukutwa na watu walokuwa wameibiwa ng’ombe.
Basi Mwanamabonde akiwa mwenyekiti wa kijiji hicho aliwaambia kuwa pamoja na ng’ombe kuwa wako kwa bwana Pandasahani, itakuwa ni vigumu au haitawezekana ng’ombe hao muwachukue hivi hivi tu.

Mzee Mwanamabonde akawaambia tulieni hapa kwanza. Basi Mwanamabonde akaitisha mkutano wa wanakijiji wake kisha wakaenda pamoja nao kwenye mji wa Pandasahani ambapo ng’ombe mbalimbali wa wizi walitunzwa hapo.

Ilikuwa ni siku Pandasahani alikuwa ameamua kufanya karamu kwani walikuta ng’ombe amechinjwa, nyama zikipikwa jikoni. Jamii iliyochoshwa na vitendo vichafu vya Pandasahani iliwaamuru wake zake Pandasahani kujitwisha vyungu vya nyama kutoka jikoni bila kujali wanaungua kiasi gani. Pandasahani aliambiwa wanapelekwa kituo cha Polisi. Wakiwa pamoja na Pandasahani na familia yote, waliongozwa hadi katikati ya pori ambako waliambiwa kuwa hapa ndiyo kituo cha Polisi.

Waliamuriwa kusali mara ya mwisho kwani siku zao zilikuwa zimekwisha. Sahani na familia yake yote kila mtu kwa wakati wake alisali. Utesaji ulipoanza kwa akina mama kwa kukatwa ziwa moja huku wakiwa hai bado. Hatimaye akina baba nao walionja joto ya jiwe kwa kukatwa sehemu za siri wakiwa hai. Kazi ya mwisho ilikuwa kuuwawa kwa familia ya Pandasahani. Maiti zao ziliachwa porini.
Baada ya kubainika mauaji haya, polisi walikuja, lakini mzee Mwanamabonde alikana akasema hajui kwani halikuwa eneo lake. Polisi wakamwacha huru.

Mzee Mwanamabonde akazuru Kahama kueneza mbinu za kuanzisha Sungunsungu. Akiwa wilayani Kahama, alikutana na mzee Kishosha, mzee Jugi na wengine walioonekana wazuri na maarufu. Aliwaelezea azma yake ya kuanzisha sungusungu. Aliwapa mbinu aliyokuwa akitumia huko kwake.

Harakati hizi za kuanzisha sungusungu zilizagaa na kutafsiriwa kuwa wanaanzisha chama cha siasa. Mkuu wa wilaya Kahama alimwarifu Rais kuwa kuna chama cha siasa kimeanzishwa Kahama. Rais aliagiza mara moja watu hao wafunguliwe na mashitaka. Kweli muda mrefu haukupita watu hawa akina mzee Jugi, mzee Kishosha na wengine wakahukumiwa kifungo cha miezi kumi kila mmoja.

Tume iliteuliwa baadaye walifanyia uchunguzi chama hiki. Katika Tume hiyo akiwemo Mbunge wa Maswa Mheshimiwa Shillingi na wengine. Katika kuwahoji wazee hao waliokuwa wakituhumiwa, Mheshimiwa Shillingi aliwataka waongee kisukuma. Wazee hawa kila mmoja alidai wamechoshwa na wezi. Hapakujitokeza suala la kisiasa hata kidogo.

Tume ikawasilisha taarifa yake kwa Mheshimiwa Rais, muda si mrefu Rais akamuru watu hao waachiliwe mara moja na waendelee kuunda sungusungu yao kwa minajili ya ulinzi wa ng’ombe wao na mali zao nyingine. Katika eneo la Lubaga sungusungu wamefanikiwa kwa kiasi kikiubwa katika utendaji wao wa kazi za kila siku na kusaidia watu kuishi katika amani na usalama.chombo bila nahodha huenda mrama ndivyo inavyokuwa sungusungu wa Lubaga wao kama wao wana utawala wao.
Hakika jeshi la jadi halikuwa na mzaha hata kidogo kwani katika utawala wake kulikuwa na Mtemi (Ntemi) ambaye alichaguliwa kwa kigezo cha kuwa na maarifa ya tiba za jadi au za asili ,na huacha madaraka kwa muda wa miaka mitatu labda aumwe,afe,ahame ndio amejivua uongozi na uongozi haufuati ukoo fulani bali huchaguliwa na wananchi wenyewe.msaidizi wake aliyeitwa Mwambilija “Mtwale”,katibu wake aliitwa mwandiki na msaidizi wake pia kuna kamamanda mkuu aliyetwa kwa jina la asili la Nsumba ntale na wajumbe wa kamati.Katika uongozi wao hawana kiongozi mwanamke kwa minajili ya kwamba wanawake hawawezi kutunza siri lakini kwa uchunguzi tulioufanya kuna matawi mengine kuna wenyeviti wanawake mfano mzuri ni katika kijiji cha Mwagala.
Katika jamii ya wasukuma kuna kuwa na penga mbili (filimbi)viongozi wa familia wanakuwa nazo yaani mama na baba popote wakitokewa na tatizo wanapiga sungusungu na watu wengine wanakuja na katibu anaandika tatizo lililotokea .
“Ndulilu”ni kipande cha kibuyu kilichotobolewa katika sehemu tatu na sehemu mbili zinazibwa sehemu moja inatumika kwa kupiga endapo tu kuna tatizo kubwa mfano wizi wa mifugo na mauwaji.
Tukumbuke kuwa ulinzi wa jadi ni sheria ndogondogo tuliojiwekea ili kujilinda na mali zetu .Endapo mtu ameenda kinyume na sheria tuliojiwekea hupewa adhabu maarufu kama kupigwa “mchenya”ambazo ni faini ndogo ndogo na ukiendelea wanakutenga (kumtulija)ina maana usishiriki katika shughuli zote za jamii ukifiwa watu wanakuja kuzika lakini sungusungu wanawafukuza ndugu zako kuwafariji na kulala matangani na ukifa utakuwa umeikomboa jamii yako.Ukiwa mjeuri,mwizi,unaharibu mazingira kwa kiasi kikubwa unapelekwa kujikomboa katika jeshi jingine na unatozwa faini kubwa Na adhabu zao haziangalii jinsi wala umri.
Kila kwenye mafanikio hakukosi kuwa na matatizo ndivyo ilivyo kwa wenzetu hawa sungusungu hawana vifaa vya ulinzi vya kisasa ,isitoshe kuna watu ambao hukutwa nyakati za usiku lakini si wezi na kwa upande wao yaani sungusungu wenyewe wanakuwa wanakiuka miiko yao kwa kuwa wanafiki na wenye majungu hivyo kukwamisha zoezi zima la ulinzi .
Licha ya hayo kuna mafanikio ambayo wameyapata ni kupungua kwa wimbi la wizi wa mifugo kwani vijana ndio hasa wenye ari na wito wa kulinda nchi yao na mali zao.
Sungusungu wanautaratibu wa usambazaji wa taarifa kwenda tawi jingine ujulikanao kama mwano ni taarifa ya hatari kutoka tawi moja kwenda jingine endapo kuna tatizo limetokea ili waweze kusaidiana kulitatua .Endapo mifugo imepatikana katika tawi jirani huwaarifu na kwenda kuchukua ,au wezi wamepatikana n.k.
Ikiwa mali imepatikana Mwenyewe asipopatikana kwa upande wa mifugo inatunzwa na kutangazwa kwenye matawi ya jirani baada ya miezi sita inakuwa ni mali ya sungusungu na fedha inayopatikana kutokana na faini au mifugo iliyookotwa hupelekwa katika ujenzi wa maendeleo kama vile shule na hospitali.
Kwa hali ilivyo sasa hivi kila mti una mwenyewe ukikutwa umekata mti unapelekwa kwa sungusungu na sungusungu wanakuhukumu.
Kwa upande wangu naona sungusungu ni wazuri katika suala zima la utunzaji wa mazingira hivyo basi sisi wananchi inabidi tuwaunge mkono sungusungu na kwa upande wao basi walegeze adhabu kwa aliyetengwa angalau aweze kushiriki katika masuala ya kidini tofauti na ilivyo sasa.

Serikali kutambua fursa hii iliyopo ya ulinzi wa jadi(sungusungu) ikizingatia suala la ulinzi shirikishi ambao umeonyesha mafanikio makubwa kwa taifa hili hususani vyombo vya ulinzi kwani jamii inachukua nafasi kubwa kama chanzo cha habari.
Mafunzo kwa taasisi za namna hii ni muhimu sana ili kuongeza ufanisi zaidi kwa kuzingatia ukweli na uwazi.

SUNGUSUNGU WATUNZA MAZINGIRA

Na.Mwantumu Jongo.
Wengi wetu tumekuwa tukifahamu kuwa sungusungu ni jina la wadudu wadogo wadogo weusi ambao hutambaa ardhini.Wadudu hawa huuma pindi wanapokandamizwa.Mtu aumwapo na wadudu hawa huisi uchungu. Neno hili lilipendekezwa litumike kwa kikundi hicho cha Usalama kwa sababu ya kujihami kwao kwa haraka wawapo na tatizo.
Licha ya kwamba sungusungu hawa adhabu zao haziendani na sheria ya nchi mfano mzuri aliyetengwa haruhusiwi katika kufanya ibada lakini wana mchango mkubwa katika kutunza mazingira yetu.

“Kutunza mazingira ni sehemu ya kazi yao “alisema bwana W.C.Mlenge.
NAFRAC ilipoanza mradi ilikuta sungusungu imeshatawazwa . Mnamo mwaka 1992 mwezi wa saba walienda Bariadi kufanya utafiti wa taasisi za kiasili zitasaidiaje katika kutunza mazingira wakaitisha mkutano wakiongozwa na chifu wao wa zamani ambaye alijua mambo ya mila na uhusiano mzuri (Mhola)Dagashida waliendesha mkutano vizuri.
Ndipo tulipooona dhahiri kuwa wahenga hawakukosea waliposema tunza mazingira nawe ya kutunze ni usemi uliokuweko toka enzi za mababu zetu sungusungu hawa waliweza kutunza mzingira yao kwa vitendo .
Toka jadi wao ndio walikuwa walinzi wa misitu ya asili hawakuishia hapo walikuwa wanalinda kisima kisichafuliwe kwa kutunza misitu ulio karibu na kisima ili kiwe na maji mengi .
sungusungu walianzisha na kuyatunza maeneo mengine ya kulishia mifugo maarufu kama ngitili hao ndio walikuwa walinzi wakuu mfano mzuri katika vijiji vya Ikonda,Busongo,Mwamishani wanataratibu zao za kutunza ngitili kwa kufanya hivyo waliweza kupunguza kulishia mifugo eneo bila ya ruhusa ya mwenye eneo hilo ukikutwa walikuwa wanakuadhibu kisheria .

Pia waliweza kutatua migogoro ya mipaka ya mashamba katika eneo lao hii ilisaidia katika jamii za kisukuma kuishi kwa amani na upendo .Sungusungu wapo katika kamati za mazingira hivyo hutoa mawazo mazuri katika utunzaji wa misitu ya asili na wao ndio watekelezaji wakuu wa suala zima la utunzaji wa mazingira.
Kuwinda ,kuchunga na kukata miti kulikatazwa kulifanywa kwa ruhusa maalum kutoka kwa mwenyekiti wa sungusungu ukikutwa unalipa faini hii ilisaidia sana jamii ya kisukuma kuweza kuwa na mazingira yaliyoboreshwa kiukamilifu.
Nilikuwa na kiu ya kujua asili hasa ya sungusungu ni nini ndipo hapo bwana mwenyekiti wa sungusungu wa Lubaga aliponielezea sungusungu ilianzishwa mwaka 1982 katika kijiji cha ng’wang’halanga wilayani Nzega. Mzee Mwanamabonde alianzishwa sungusungu baada ya kukutwa na watu walokuwa wameibiwa ng’ombe.
Basi Mwanamabonde akiwa mwenyekiti wa kijiji hicho aliwaambia kuwa pamoja na ng’ombe kuwa wako kwa bwana Pandasahani, itakuwa ni vigumu au haitawezekana ng’ombe hao muwachukue hivi hivi tu.

Mzee Mwanamabonde akawaambia tulieni hapa kwanza. Basi Mwanamabonde akaitisha mkutano wa wanakijiji wake kisha wakaenda pamoja nao kwenye mji wa Pandasahani ambapo ng’ombe mbalimbali wa wizi walitunzwa hapo.

Ilikuwa ni siku Pandasahani alikuwa ameamua kufanya karamu kwani walikuta ng’ombe amechinjwa, nyama zikipikwa jikoni. Jamii iliyochoshwa na vitendo vichafu vya Pandasahani iliwaamuru wake zake Pandasahani kujitwisha vyungu vya nyama kutoka jikoni bila kujali wanaungua kiasi gani. Pandasahani aliambiwa wanapelekwa kituo cha Polisi. Wakiwa pamoja na Pandasahani na familia yote, waliongozwa hadi katikati ya pori ambako waliambiwa kuwa hapa ndiyo kituo cha Polisi.

Waliamuriwa kusali mara ya mwisho kwani siku zao zilikuwa zimekwisha. Sahani na familia yake yote kila mtu kwa wakati wake alisali. Utesaji ulipoanza kwa akina mama kwa kukatwa ziwa moja huku wakiwa hai bado. Hatimaye akina baba nao walionja joto ya jiwe kwa kukatwa sehemu za siri wakiwa hai. Kazi ya mwisho ilikuwa kuuwawa kwa familia ya Pandasahani. Maiti zao ziliachwa porini.
Baada ya kubainika mauaji haya, polisi walikuja, lakini mzee Mwanamabonde alikana akasema hajui kwani halikuwa eneo lake. Polisi wakamwacha huru.

Mzee Mwanamabonde akazuru Kahama kueneza mbinu za kuanzisha Sungunsungu. Akiwa wilayani Kahama, alikutana na mzee Kishosha, mzee Jugi na wengine walioonekana wazuri na maarufu. Aliwaelezea azma yake ya kuanzisha sungusungu. Aliwapa mbinu aliyokuwa akitumia huko kwake.

Harakati hizi za kuanzisha sungusungu zilizagaa na kutafsiriwa kuwa wanaanzisha chama cha siasa. Mkuu wa wilaya Kahama alimwarifu Rais kuwa kuna chama cha siasa kimeanzishwa Kahama. Rais aliagiza mara moja watu hao wafunguliwe na mashitaka. Kweli muda mrefu haukupita watu hawa akina mzee Jugi, mzee Kishosha na wengine wakahukumiwa kifungo cha miezi kumi kila mmoja.

Tume iliteuliwa baadaye walifanyia uchunguzi chama hiki. Katika Tume hiyo akiwemo Mbunge wa Maswa Mheshimiwa Shillingi na wengine. Katika kuwahoji wazee hao waliokuwa wakituhumiwa, Mheshimiwa Shillingi aliwataka waongee kisukuma. Wazee hawa kila mmoja alidai wamechoshwa na wezi. Hapakujitokeza suala la kisiasa hata kidogo.

Tume ikawasilisha taarifa yake kwa Mheshimiwa Rais, muda si mrefu Rais akamuru watu hao waachiliwe mara moja na waendelee kuunda sungusungu yao kwa minajili ya ulinzi wa ng’ombe wao na mali zao nyingine. Katika eneo la Lubaga sungusungu wamefanikiwa kwa kiasi kikiubwa katika utendaji wao wa kazi za kila siku na kusaidia watu kuishi katika amani na usalama.chombo bila nahodha huenda mrama ndivyo inavyokuwa sungusungu wa Lubaga wao kama wao wana utawala wao.
Hakika jeshi la jadi halikuwa na mzaha hata kidogo kwani katika utawala wake kulikuwa na Mtemi (Ntemi) ambaye alichaguliwa kwa kigezo cha kuwa na maarifa ya tiba za jadi au za asili ,na huacha madaraka kwa muda wa miaka mitatu labda aumwe,afe,ahame ndio amejivua uongozi na uongozi haufuati ukoo fulani bali huchaguliwa na wananchi wenyewe.msaidizi wake aliyeitwa Mwambilija “Mtwale”,katibu wake aliitwa mwandiki na msaidizi wake pia kuna kamamanda mkuu aliyetwa kwa jina la asili la Nsumba ntale na wajumbe wa kamati.Katika uongozi wao hawana kiongozi mwanamke kwa minajili ya kwamba wanawake hawawezi kutunza siri lakini kwa uchunguzi tulioufanya kuna matawi mengine kuna wenyeviti wanawake mfano mzuri ni katika kijiji cha Mwagala.
Katika jamii ya wasukuma kuna kuwa na penga mbili (filimbi)viongozi wa familia wanakuwa nazo yaani mama na baba popote wakitokewa na tatizo wanapiga sungusungu na watu wengine wanakuja na katibu anaandika tatizo lililotokea .
“Ndulilu”ni kipande cha kibuyu kilichotobolewa katika sehemu tatu na sehemu mbili zinazibwa sehemu moja inatumika kwa kupiga endapo tu kuna tatizo kubwa mfano wizi wa mifugo na mauwaji.
Tukumbuke kuwa ulinzi wa jadi ni sheria ndogondogo tuliojiwekea ili kujilinda na mali zetu .Endapo mtu ameenda kinyume na sheria tuliojiwekea hupewa adhabu maarufu kama kupigwa “mchenya”ambazo ni faini ndogo ndogo na ukiendelea wanakutenga (kumtulija)ina maana usishiriki katika shughuli zote za jamii ukifiwa watu wanakuja kuzika lakini sungusungu wanawafukuza ndugu zako kuwafariji na kulala matangani na ukifa utakuwa umeikomboa jamii yako.Ukiwa mjeuri,mwizi,unaharibu mazingira kwa kiasi kikubwa unapelekwa kujikomboa katika jeshi jingine na unatozwa faini kubwa Na adhabu zao haziangalii jinsi wala umri.
Kila kwenye mafanikio hakukosi kuwa na matatizo ndivyo ilivyo kwa wenzetu hawa sungusungu hawana vifaa vya ulinzi vya kisasa ,isitoshe kuna watu ambao hukutwa nyakati za usiku lakini si wezi na kwa upande wao yaani sungusungu wenyewe wanakuwa wanakiuka miiko yao kwa kuwa wanafiki na wenye majungu hivyo kukwamisha zoezi zima la ulinzi .
Licha ya hayo kuna mafanikio ambayo wameyapata ni kupungua kwa wimbi la wizi wa mifugo kwani vijana ndio hasa wenye ari na wito wa kulinda nchi yao na mali zao.
Sungusungu wanautaratibu wa usambazaji wa taarifa kwenda tawi jingine ujulikanao kama mwano ni taarifa ya hatari kutoka tawi moja kwenda jingine endapo kuna tatizo limetokea ili waweze kusaidiana kulitatua .Endapo mifugo imepatikana katika tawi jirani huwaarifu na kwenda kuchukua ,au wezi wamepatikana n.k.
Ikiwa mali imepatikana Mwenyewe asipopatikana kwa upande wa mifugo inatunzwa na kutangazwa kwenye matawi ya jirani baada ya miezi sita inakuwa ni mali ya sungusungu na fedha inayopatikana kutokana na faini au mifugo iliyookotwa hupelekwa katika ujenzi wa maendeleo kama vile shule na hospitali.
Kwa hali ilivyo sasa hivi kila mti una mwenyewe ukikutwa umekata mti unapelekwa kwa sungusungu na sungusungu wanakuhukumu.
Kwa upande wangu naona sungusungu ni wazuri katika suala zima la utunzaji wa mazingira hivyo basi sisi wananchi inabidi tuwaunge mkono sungusungu na kwa upande wao basi walegeze adhabu kwa aliyetengwa angalau aweze kushiriki katika masuala ya kidini tofauti na ilivyo sasa.

Serikali kutambua fursa hii iliyopo ya ulinzi wa jadi(sungusungu) ikizingatia suala la ulinzi shirikishi ambao umeonyesha mafanikio makubwa kwa taifa hili hususani vyombo vya ulinzi kwani jamii inachukua nafasi kubwa kama chanzo cha habari.
Mafunzo kwa taasisi za namna hii ni muhimu sana ili kuongeza ufanisi zaidi kwa kuzingatia ukweli na uwazi.

UZURI NA UBAYA WA MWAROBAINI

Na.Mwantumu Jongo.
Hakika uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti; kwa kweli wahenga hawakukosea waliposema usemi huo unadhihirika katika huu mti wa mwarobaini kutokana na umaarufu wake kuwa unatibu maradhi mengi ndipo hapo watu wengi walipoupanda kwa wingi katika maeneo yao kwa kutarajia faida zaidi bila kuangalia upande wa pili wa shilingi kwani sasa mti huu imegundulika ukiupanda karibu na matunda basi matunda yako yatakuwa machungu.

Katika eneo la shinyanga ng’warobaini uliingia katika miaka ya 1980 na wenyeji wa mkoa huu waliuita katika lugha ya kisukuma waliupenda na wakaupa kipaumbele katika kuupanda kwani ulistahamili hali ya ukame ukipanda miche ya miarobaini kumi miwili tu ndio inakufa hali hii iliwasaidia sana kutunza mazingira yao hivyo waliipanda miarobaini kwa wingi.

Kweli kizuri hakikosi kasoro ndivyo ilivyokuwa kwa mwarobaini kwani baadhi ya watu waliuchanganya mti huu wa mwarobaini na mazao yao kama vile mapapai,mapera,machungwa na hata kisamvu ikagundulika mazao hayo yaliopandwa karibu na mwarobaini matunda yake hupoteza ladha halisi kwani huwa ni machungu na uchungu wake hutofautiana na umbali wake na mti huu wa mwarobaini ukiwa karibu uchungu wake unaongezeka na ukiwa mbali kidogo uchungu wake unapungua kidogo.

Hali hii iliwasikitisha sana wakazi wa Shinyanga kwani hata mimea inayotambaa inayopandwa karibu na miarobaini hufa haraka kwa sababu ya ushindani unaokuwepo wa maji na virutubisho. Mti huu uwa na hali ya ukijani wa muda wote wa mwaka mzima Habari hizi zikafika mahali pake na sipengine bali ni katika kituo cha uendelezaji misitu asilia na kilimo mseto(NAFRAC) .
Kwa kipindi kile wataalamu wa HASH/ICRAF( kwa sasa NAFRAC) walifanya jaribio dogo la kiuchunguzi lililohusisha miti minne nayo ni Acacia polyacantha kwa lugha ya Kiswahili hujulikana kama migu ,Albizia lebbeckk-Alibizia,,Acacia nilotica(mihale), Azedractha indica (neem), ambao ndio huu mwarobaini tunaoupanda katika maeneo yazungukayo maeneo yetu.

Jaribio hili lilikuwa na lengo la kujua uhusiano uliopo katika ya miti hii hasa athari zinazojitokeza juu ya ardhi na chini ya ardhi pia kiwango cha kemikali ipatikanayo. .Miti hii ilipandwa ikiwa imechanganywa na mazao ya kilimo hususani mahindi. Katika mavuno ukilinganisha miti yote iliyofanyiwa uchunguzi, mavuno ya mahindi na upimaji vilifanyika karibu ya mti na katikati ya mti isipokuwa katika migu chini ya kivuli cha mti huu aina ya migu mavuno yalikuwa hafifu tofauti na miti mingine ambapo mavuno hayakuonyesha tofauti yoyote.Ila iligundulika kuwa mizizi ya mwarobaini huenda mbali zaidi kutafuta maji na virutubisho hii wakati mwingine husababisha kupasua nyufa za nyumba na ardhi.

“Wakati tunaanzisha bustani ya miche ya miti tuliweka kinga upepo (wind break) ili kukinga miche isiharibiwe na upepo mkali tulipanda miche ya miarobaini na matunda ndani ya msimu mmoja lakini cha ajabu miti ya matunda ilikufa. Tulifanya jaribio linalohusisha miarobaini na mazao mengine kama mahindi , yalistawi vizuri bila tatizo lolote.
Jaribio la pili lilifanywa kwa kuotesha miche ya miti ya matunda na kuipanda katikati ya mistari miwili ya mwarobaini kwa kutofautisha umbali wa mita tatu ,tano na nane matokeo ya jaribio hilo ni kwamba miti iliyokuwa karibu ilikufa na iliyokuwa mbali matunda yake yalikuwa na ukakasi hayaliki kwani yalikuwa machungu na hadi sasa kuna mchungwa mmoja ambao upo lakini hauzai matunda miti iliyojaribu kuweka matunda uchungu wake ulitofautiana kulingana na umbali wake na mwarobaini.
Uzoefu unaonyesha kuwa jamii ya wakazi wa mkoa wa shinyanga wana utamaduni wa kuacha miti ya asili mashambani ambayo imekuwa ikisifiwa kutokuwa na madhara makubwa katika mazao ya kilimo.
Hakika sasa wakati umefika wa watafiti kufanya uchunguzi zaidi kuhusiana na suala hili ili tuweze kujua tukihamasisha wananchi kupanda miti ya kigeni(mwarobaini basi tuwe tunawashauri wasichanganye na matunda ya biashara na hata kuupanda karibu na nyumba zao. “Tuzingatie elimu asilia”

WANAWAKE NA MIFUKO YA LAMBO

Na.Mwantumu Jongo.
Ni siku nyingine tena naamka asubuhi na mapema nikiwa napiga mswaki nikijiandaa kwenda kazini .Moshi mzito umetanda angani wengi wetu wenye afya mgogoro tulikuwa ndipo nilipotazama upande wa kulia kwangu kuona mama anachoma moto mifuko ya plastiki .
Hali hii ndiyo iliyonipelekea nishike kalamu yangu na kuandika kero niliyokumbana nayo na athari zake kwa binadamu ila leo nitazungumzia mwanamke kwa undani zaidi .
Kutokana na utafiti unaoonyesha kuwa mwanamke ndiye anaye tumia mifuko ya plastiki kwa kiwango kikubwa lakini kulingana na mila na desturi zetu za kiafrika tunaamini kuwa asilimia kubwa ya kinamama ndiyo huenda kununua bidhaa mbalimbali za nyumbani kitendo cha kuwepo kwa mifuko ya palstiki kunafanya wanawake wengi kutokuwa na utamaduni wa kubebea vikapu kwa ajili ya kubebea bidhaa wanazozinunua.

Kutokana na utandawazi hali hii imekuwa tofauti na enzi za mababu zetu ambapo mwanamke ndiye alikuwa anakwenda sokoni gengeni kununua mahitaji ya nyumbani lakini hivi sasa hali imekuwa tofauti kidogo wengi wanasema kutokana na usomi ,utandawazi na sayansi na teknolojia na uelewa wa haki sawa kwa wote hata wanaume nao wanahusika na matumizi ya mifuko ya plastiki.

Uchafuzi wa mazingira umekuwa tishio kwa maendeleo ya Taifa hivyo yanahitaji matumizi endelevu ya mazingira kwa ajili ya kizazi kijacho pamoja na kuwepo kwa madhara ya kimazingira pia kuna madhara ya kiafya kwa wanawake wengi kwakutojua athari wanazopata kwa kuchoma mifuko ya lambo.

Kwa upande wa wanawake athari wanazopata kutokana na kuchoma mifuko ya lambo moshi wake akiuvuta huziba njia za uzazi na kujifungua kabla ya wakati ikiwa ni chanzo kikubwa ni kuvuta moshi unaotokana na mifuko ya plastiki zilizochomwa hivyo kusababisha foleni za wanawake wengi kwenda hospiatli hata kwa waganga kwa sababu ya kutopata watoto au watoto wao kufa kumbe wachawi wakubwa ni wao wenyewe wanachafua mazingira yao.

Hata hivyo kwa upande wa wakinamama wajawazito mtoto anaweza kufia tumboni au kuzaliwa akiwa na na upungufu wa uzito (njiti) kwani kwa kawaida mtot huzaliwa akiwa na kilo …….

Ingawa mtoto wa mwanamke huyo huweza kupata matatizo ya kukua au mtindio ubongo pamoja na maradhi ya Saratani ya damu jambo ambalo litamchukua muda mama huyu katika kuhakikisha afya ya mtoto wake inatengemaa .

Ikiwa matatizo yote hayo yanamkabili mwanamke kutokana a na athari za matumizi na uchomaji wa mifuko ya lambo ni wajibu wa mwanamke kuwa mstari wa mbele kupiga vita matumizi ya mifuko ya lambo(plastiki)badala yake kuwa mstari wa mbele katika matumizi ya vikapu vya asili kwa ajili ya kubebea mahitaji mbalimbali ya nyumabani .

Naamini suala la kuacha kutumia mifuko ya plastiki likitekelezeka tatizo la uharibifu wa mazingira unaotokana na mifuko ya plastiki litamalizika .Lakini ni jambo la busara kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali pamoja na baraza la Taifa la uitunzaji mazingira nchini (NEMC) katika suala zima la kuelimisha juu ya umuhimu wa kutunza mazingira ni vyema jamii yote inayoelimishwa ikashiriki kikamilifu katika kupiga vita uharibifu wa mazingira unaotokana na chanzo chochote kile .

Hivyo ningependa kutoa changamoto kuwa wanawake wasijirudishe nyuma ni dhamana waliyopewa ya kuwa mstari wa mbele katika kutunza mazingira kwa kutumia vikapu waitekeleze kwa kwa jitihada zote isiwe nguvu ya soda bali iwe endelevu kwa manufaa ya kizazi kijacho na jamii kwa ujumla.

NJIA SAHIHI YA KUOKOA MAEMBE

Na.Mwantumu Jongo


Nzi wa embe ambaye kwa jina la kitaalamu hujulikana kama Bactrocera dorsalis hufanana na nzi wengine wanaoshambulia embe na matunda mengine .Nzi huyu hutofautishwa na nzi wengine kirahisi kwa umbo lake linalofanana na lile la manyigu na opia ana alama ya T mgongoni mwake .Nzi huyu hutaga mayai mengi ndani ya embe na kusababisha embe kuoza na kuanguka chini kwa wingi .Inzi huyu ameonekana nchini kwa mara ya kwanza mwezi Desemba 2003.

ATHARI ZA INZI WA EMBE
Nzi huyu anatoboa na kutaga mayai mengi ndani ya embe hali ambayo husababisha kupungua kwa ubora wa embe .Funza anayejitokeza baada ya mayai kuanguliwa huishi kw a kula nyama ya embe .Hali hii husababisha vidonda ndani ya embe na matokeo yake ni kuoza kwa embe na kuanguka chini uharibifu huu hufikia kati ya asilimia 50-80 ya matunda yote yanayozaliwa.Athari kubwa ipatikanayo kwa kuwepo nzi huyu wa embe hapa nchini ni uwezekano wa kukosa soko la kimataifa kwa embe na matunda mengine tunayozalisha hapa nchini.

UDHIBITI WA NZI WA EMBE
Okota mara kwa mara na fukia embe na matunda mengine yaliyoanguka chini kwa kina cha futi tatu.Palilia mara kwa mara eneo lililoko chini ya mwembe ili kutoa wazi funza na buu wa inzi wa emebe kwa wadudu walawangi na pia waathirike na hali mbaya ya hewa kwa ukuaji wao.

Tumia kivutia wadudu (pheromone aina ya methyleugenol)iliyochanganywa na kiuatilifu cha kuua wadudu dichlorovos ili kuua madume wa nzi na hivyo kupunguza idadi yao.

Tumia mbinu husishi za IPM yaani tumia michanganyiko wa mbinu zote katika utaratibu unaofaa na ili kuongeza udhibiti wa nzi huyu.Nyunyiza viatilifu vilivyokwisha nguvu haraka kwa kufuata ushauri wa bwana shamba katika miti ambayo ina nzi wengi .Udhibiti uanze mapema wakati miembe inapoanza kutoa maua.

HATUA ZA VVU KATIKA MWILI WA BINADAMU

Na.Mwantumu Jongo.
Katika mwili wa binadamu ni muhimu sana kwa kila mmoja wetu kupima damu kujua kama unaishi na Virusi vya UKIMWI(VVU) au la kuna hatua tatu tofauti za VVU.

UNA VVU UNA AFYA NZURI.
Katika hatua hii inamaanisha kuwa mfumo wako wa kinga mwilini uko imara na idadi ya CD4 zako ziko juu huhitaji kutumia dawa za kupunguza makali ya vvu (ARV)kama ni mzazi waandae watoto wako kwa kuwaeleza kuhusu VVU .Hakikisha wataangaliwa vizuri pindi utakapozidiwa na ugonjwa au utakapofariki .Tafuta msaada wa kukusaidia kukabilia
na na hali hii.

UNA VVU NA UMEZIDIWA NA UKIMWI
katika hatua hiii unagua sana mara kwa mara hupati nafuu .Inamaanisha kwamba mfumo wako wa kinga ndio dhaifu sana lazima upate matibabu kwa magonjwa yako ambayo hushambulia mwili wakati kinga imepungua huitwa magonjwa nyemelezi shauriana na muhudumu wa afya kuhusu kuanza kutumia ARV. Kwa kawaida watu hufuata matibabu wakati wakiwa wagonjwa na hawajiwezi na kama unatunza mgonjwa na anatumia ARV hakikisha unaelewa vizuri kuhusu dawa hizo zungumza na muhudu wa afya kwa maelezio zaidi .

UNA VVU NA UNAANZA KUUMWA
Katika hatua hii mfumo wako wa kinga unaanza kuwa dhaifu muombe muhudumu wa afya akupime idadi ya CD4 kwenye damu yako .Hii itakuwezesha kufahamu kuanza kutumia ARV .Magonjwa unayoyapata unapokuwa na VVU yanaweza kutibika lakini lazima uwe mwangalifu kwa sababu baadhi ni magonjwa hatari ni muhimu kwenda hospitali hospitali.

MAONI
Mgonjwa ahakikishe akishajua kama ameathirika na Virusi vya UKIMWI ahakikishe anapata ushauri nasaha na kuwahi kutumia dawa za ARV kwani kwa kufanya hivyo kutamsaidia mgonjw ahuyo kuongeza muda wake wa kuishi .
Katika mwili wa binadamu ni muhimu sana kwa kila mmoja wetu kupima damu kujua kama unaishi na Virusi vya UKIMWI(VVU) au la kuna hatua tatu tofauti za VVU.

UNA VVU UNA AFYA NZURI.
Katika hatua hii inamaanisha kuwa mfumo wako wa kinga mwilini uko imara na idadi ya CD4 zako ziko juu huhitaji kutumia dawa za kupunguza makali ya vvu (ARV)kama ni mzazi waandae watoto wako kwa kuwaeleza kuhusu VVU .Hakikisha wataangaliwa vizuri pindi utakapozidiwa na ugonjwa au utakapofariki .Tafuta msaada wa kukusaidia kukabilia
na na hali hii.

UNA VVU NA UMEZIDIWA NA UKIMWI
katika hatua hiii unagua sana mara kwa mara hupati nafuu .Inamaanisha kwamba mfumo wako wa kinga ndio dhaifu sana lazima upate matibabu kwa magonjwa yako ambayo hushambulia mwili wakati kinga imepungua huitwa magonjwa nyemelezi shauriana na muhudumu wa afya kuhusu kuanza kutumia ARV. Kwa kawaida watu hufuata matibabu wakati wakiwa wagonjwa na hawajiwezi na kama unatunza mgonjwa na anatumia ARV hakikisha unaelewa vizuri kuhusu dawa hizo zungumza na muhudu wa afya kwa maelezio zaidi .

UNA VVU NA UNAANZA KUUMWA
Katika hatua hii mfumo wako wa kinga unaanza kuwa dhaifu muombe muhudumu wa afya akupime idadi ya CD4 kwenye damu yako .Hii itakuwezesha kufahamu kuanza kutumia ARV .Magonjwa unayoyapata unapokuwa na VVU yanaweza kutibika lakini lazima uwe mwangalifu kwa sababu baadhi ni magonjwa hatari ni muhimu kwenda hospitali hospitali.

MAONI
Mgonjwa ahakikishe akishajua kama ameathirika na Virusi vya UKIMWI ahakikishe anapata ushauri nasaha na kuwahi kutumia dawa za ARV kwani kwa kufanya hivyo kutamsaidia mgonjw ahuyo kuongeza muda wake wa kuishi .

CHANJO YA PEPOPUNDA KWA WANAWAKE

Na.Mwantumu Jongo.
Pepopunda ni ugonjwa wa hatari unaoambukiza na bacteria ambao huingia mwilini kupitia kwenye kidonda au jeraha .Ugonjwa huu huwapata watu wa rika zote .chanjo ya pepopunda kwa wanawake kila mwanamke kuanzia umri wa miaka kumi na tano na arobaini na nne ni muhimu akamilishe chanjo dhidi ya pepopunda .

Katika sehemu nyingi duniani wanawake hujifungua katika mazingira machafu hii inamuweka mama na mtoto katika hali ya kupata ugonjwa wa pepopunda ambao huuua watoto wachanga wengi kama mama hakupata chanjo ya pepopunda mtoto azaliwaye ni rahisi kuupata ugonjwa huu.

Vijidudu vya ugonjwa wa pepopunda huzaliana kwenye majiraha machafu hii inaweza kutokea ikiwa kiwembe kisu kichafu kitatumika kukatia kitovu cha mtoto au kitu chochote kichafu kikiwekwa kwenye kitovu cha mtoto mchanga .kitu chochote kinachotumika kukatia kitovu cha mtoto ni sharti kwanza kioshwe au kiunguzwe kwenye moto na baadae kuachwa kipoe.

Wanawake wote wanaofikia umri wa kuzaa wapate chanjo dhidi ya pepopunda wanawake wajawazito wahakikishe kuwa wamepata chanjo hizo na kwa namna hiyo mama na mtoto atakayemzaa atakuwa amepata kinga dhidi ya ugonjwa huu.kama mamajamzito hajawahi kuchanjwa apewe chanjo ya pepopunda mara moja chanjo ya pili itolewe wiki nne baadae chanjo ya tatu miezi sita baadaya chanjo ya pili chanjo ya nne nay a tano zitolewe mwaka mmoja baada ya ile iliyotangulia ikiwa mwanamke amepata chanjo ya ugonjwa huu maratano atakuwa amepata kinga dhidi ya ugonjwa huu katika umri wake wote wa kuweza kuzaa .na mtoto atakuwa amekingwa na ugonjwa wa Pepopunda.
Shime wakinamama hakikisheni mnapatiwa chanjo hii kwa usahihi na serikali iwe mstari wa mbele katika kusogeza huduma hii karibu na wananchi ili kupunguza idadi ya vifo vya kinamama na watoto.
ATHARI ZIPI HUPATIKANA KWA KUTOMNYONYESHA MTOTO
Wakinamama wa kisasa wameibua tabia ya kutotaka kuwanyonyesha watoto wao maziwa ya mama kwa kuhofia kupoteza uhalisia wa matiti yao eti kwa kile kinachoitwa kulegea na hivyo kupoteza umbo lake la awali.Hali hii imekuwa ikienea kwa kasi katika jamii nyingi na kuchangia kasi ya ongezeko la vifo vya watoto wachanga na watoto kuanzia umri wa miaka miwili hadi mitano.

Ingawa hata wale wanawake wengi wanaonyonyesha , hawanyonyeshi inavyotakiwa hali hii inatokana na sababu nyingi kwa mfano desturi ya kulikiza mapema ,kukosa
wa kunyonyesha kwa sababu ya kazi nyingi na fikra potofu zinazowafanya wanawake wasinyonyeshe kama vile kuamini mama akiwa mjamzito asinyonyeshe au mtoto akiharisha hatakiwi kunyonyeshwa.


Kumnyonyesha mtoto maziwa ya mama ni muhimu sana kwa afya bora na ukuaji wake hii inatokana kwamba maziwa ya mama ni chakula kilicho salama na chenye virutubisho vyote ubora wa maziwa ya mama kwa mtoto anapozaliwa hadi kufikia miezi minne chakula chake kikuu ni maziwa ya mama maziwa hayo ndio chakula ambacho pekee bora ambacho mtoto anaweza kupewa.

Ubora wa maziwa ya mama unatokana na maziwa ya mama kuwa ndio mlo pekee salama na wenye virutubisho vyote ,maziwa ya mama yanasaidia kumkinga mtoto asipate magonjwa kama vile kuharisha ,kifua na surua.Maziwa ya mama ni rahisi hayana gharama na yako tayari kwa wakati wowote na isitoshe yana maji ya kutosha kwa mahitaji ya mtoto.

Mama huanza kunyonyesha mtoto mara tu baada ya kuzaliwa maziwa ya mwanzo ni muhimu sana kwasababu yana virutubisho na viini vya kinga ya asili kwa magonjwa na wataalamu wa afya wanasisitiza kuwa maziwa haya yasikamuliwe na kumwagwa kama watu wengine wanavyofikiria kuwa maziwa haya yana madhara kutokana na rangi yake.

Mtoto baada ya kuzaliwa anyonyweshe maziwa asipewe kinywaji cha aina yeyote ,anyonyeshwe maziwa ya mama tu mpaka atakapofikia miezi minne. Wakati wa kunyonyesha mama anatakiwa kuzingatia mambo mengine muhimu anawe mikono na kuosha matiti kabla ya kumnyonyesha mtoto ,anyonyeshe akiwa amekaa ametulia ,amwekee mtoto chuchu yote mdomoni na kumshikiria titi .Kila wakati mama anaponyonyesha mtoto anyonyeshe matiti yote mawili,amnyonyeshe mtoto mpaka ashibe kabisa,amtoe mtoto hewa kwa kumweka begani na kumsugua taratibu mara baadaya kunyonya.

Kunyonyesha maziwa ya mama kuna faida nyingi kwa mtoto na hata kwa mama mwenyewe kwani kunasababisha maziwa ya mama kutoka hivyo kumwezesha mtoto kuendelea kunyonya na kushiba vizuri,humkinga dhidi ya magonjwa mengi ya hatari,humsaidia mama asipate ujauzito endapo mama hatakuwa anapata siku zake za hedhi hasa katika kipindi cha miezi sita toka ajifungue , kunyonyesha kunazuia matiti kujaa na kuuma ,hurudisha viungo vya uzazi katika hali yake ya kawaida

Matatizo yanayoweza kusababisha mtoto asinyonye vizuri ni pamoja na mtoto kutopakatwa vizuri,chuchu za mama zikiwa na vidonda au fupi na hata kuzimeziba , mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati wake (njiti),mtoto mwenye kilema cha mdomo na lishe duni kwa mama hivyo maziwa hayatoshi.

Tatizo hili huwakuta wakinamama wanaojifungua kwa mara ya kwanza kinachotakiwa mama azivute chuchu mara kwa mara hadi zitakapotoka kiasi cha kutosha kwa upande wa mtoto njiti au mwenye kilema anatakiwa mama amkamulie maziwa kwenye chombo na amnyonyeshe mtoto.Kwa mama mwenye chuchu zenye vidonda asafishe chuchu na amkamulie na ahakikishe kuwa anasafisha chuchu mara kwa mara.

Wajibu wa serikali ni kuandaa na kuratibu shughuli za kuelimisha jamii juu ya unyonyeshaji maziwa ya mama kwani kunyonyesha maziwa ya mama ni muhimu sana kwa ukuaji na maendeleo ya mtoto .Maisha ya watoto wengi yangeokolewa kama kinamama wangenyonyesha vizuri watoto wao ipasavyo watoto wengi nchini hawanyonyeshwi vizuri kwa sababu nyingi baadhi ya sababu hizo ni kinamama kuelemewa na kazi nyingi na hivyo kukosa muda wa kunyonyesha pia jamii kukosa elimu ya unyonyeshaji na kuwepo kwa baadhi ya mila na destuli zinazoathiri unyonyeshaji .katika kuboresha unyonyeshaji juhudi zaidi ziwekwe katika sababu zinazowafanya wakinamama wasinyonyeshe.

QUARTERLY REPORT FOR MAARIFA CENTRE-SHINYANGA

ARID LANDS INFORMATION NETWORK
P.O BOX 10098, 00100 NAIROBI


QUARTERLY REPORT FOR MAARIFA CENTRE (MARCH-JUNE 2008)


BY

MWANTUMU JONGO
COMMUNITY INFORMATION VOLUNTEER

SHINYANGA -TANZANIA



MARCH 2008








Introduction
This is a report on Community Knowledge Centre(CKC) particularly “Maarifa centre” from March to June 2008. It discusses and highlights the activities carried out on the quarterly basis.

The CKC
Maarifa centre is a Community Knowledge Centre open to the public for six days in a week (Monday to Saturday). A tally indicator tool is used to determine the number and gender of people who visited the CKC each day and what they needed in terms of services- get info, read materials e.t.c


Activities undertaken in the quarter (March-June 2008)

WORKSHOP
During the month of April 2008 workshop was organized by ALIN inorder to instil knowledge to CIV Knowledge facilitatators understand ALIN networking concept, to learn new skills on use of appropriate ICTs information and to expose and train volunteers in integrated approaches to information monitoring and evaluation. This workshop took place at Kitui / KEFRI attended by 21 Community Information Volunteers and Knowledge facilitatators. I attended and presented a detailed report with suggestions to how CIVs can monitor their activities at the CKCs.

ORIENTATION TO NAFRAC
Soon after my arrival, I was introduced to NAFRAC and its departments for the purpose of getting more information about NAFRAC how it works. Through the orientation I came to know there are four departments that include, Administration, Documentation and dissemination, Research and development and Capacity Building and community empowerment. This enabled me to work properly in order to achieve my daily work. Also I participated in mobilization and motivating departments to give out information to the community and other stakeholder’s.also to raise awareness, conduct consultations and establish baselines informations. To date, some of the staff has promised to write articles.
Also orientation extended to radio FARAJA and SIBUKA management.


ORIENTATION TO DEPARTMENT OF AGRICULTURE AND LIVESTOCK
The process has beared fruits;it has is easened the task to get information from these groups and they have created articles of their of their own,, a good example Mr. A. A. Chuwa he wrote “Rice Irrigation scheme at Bugweto” They said that earlier there was no sound coordination between members of focal groups and CIV. Currently it is easy to submit an article when we recognize and they promised me to give out information .They request for the baobab newslettesr as early as possible in order to meet their requirement.

Meeting to strengthen Focal Group
Through out this period my intension has been to attain the target as early as possible and to formulate a new focal groups near to Maarifa centre which include farmers, media press, student at primary school level and o-level and advanced student ,colleges and workers this enable me to give out local information’s. Introduce 5 new one focal Groups at chibe village which consist a farmers called Juhudi and Maarifa, mwagala consist a women small scale agriculture based on drip irrigation called and Shinyanga Municipal Council which include extension officer.


ICT training
One training was done within march-June 2008. 1female and 4 males received training on Microsoft power point appllication and can now use this program. Follow up is underway to assess the impact of the activity. More people were interested to be taught on ICTS . Henceforth 3 focal groups were enlighted on how to operate and download informations from world space and how to write an article inorder to raise an interest on shared information.
The groups were from Lubaga (Safina njema), Mwagala and Chibe village


Recruiting ALIN members
80 people were recruited to the ALIN network. 35 female and 45 male.

Information gathering/ articles creation

In the last quarter, I have generated a total of 80 articles on various livelihood issues. However, the quarter was too involving as I had a meeting to plan on, Health education campaigns and video clips to do in addition to managing the information centre.
In the CKC’s I tried on my level best to look for Kiswahili books and other reading materials from different partners like REPOA,FEMINA,ZAIN . Furthermore I managed to collect materials on Sera ya madini, Sera ya Taifa,Sera ya kudhibiti UKIMWI, Sera ya Mazingira,Sheria inayolinda uonevu dhidi ya wanawake ,Sheria ya mirathi na wosia, ukweli kuhusu Kichocho and and books like that Juma na Kichocho and watu na miti .10 different types of brochures which emphasize a knowledge based. 2 Newsletter of TATEDO and Misitu ni Mali. Also I developed and introduced a game for children when they attend its becomes easy to entertain and make an habit to ready.




Information dissemination
2 brochures of TAFORI and Maarifa were printed and distributed. Also participated to upgrade NAFRAC news letter and Maarifa –habari ni nguzo through information collection and design, articles up to now Maarifa Centre had not received any copy of the Baobab but 80 articles disseminated in the quarter with expressed satisfaction to the information.
Health=15, Environment=10 Traditions=15, Agriculture=30 , News=6, Projects=4
I conducted a case studies on good and bad practices on KICK and send to ALIN.
IMPACT ASSESMENT STUDY
Participated in an impact assessment study undertaken in Shinyanga by ALIN in collaboration with its partners during the week of 13th to 17th September 08. The main objective of this study was to test a set of key indicators developed by NOVIB partner organizations to measure changes in peoples lives to which their work contributes over a longer term period. ALIN is regarded as one of the NOVIB partners and therefore chose to undertake this study in Shinyanga because of the long term relationship and the many info exchange activities they had partnered in implementation. In this regard, I was requested to support in undertaking this activity. Questionnaires were administered and at least more than 100 community members responded actively.


MEDIA RELATIONS AND NETWORKING.

Informal and formal way of sharing and exchanging experience has been part of my approach.

Generating information, processing and making presentation through various media. Eg Radio faraja………………& Radio Sibuka.( Stories generated includes…Ijue Maarifa Centre, Mirathi na wosia, Afya ya Kinywa na Meno,usafi wa mazingira na afya ya mtu binafsi, Upatikanaji wa maji safi na salama,and ijue sheria ya Ardhi

I attended a workshop conducted at Mazingira centre which included a Shinyanga Press club on how to write an a article which was facilitated by SNV and Media Tanzania council.(MTCL)
Also I attended a workshop conducted with a TAWLAE(Tanzania women Association ) which work with legal and Paralegal in collaboration with a Shinyanga Municipal Council Management. I participated in celebration for elder people invited by TAWLAE and HELP AGE International the main theme was on “right for elder people” Old is gold.
.

During documentation process of Mazingira day exhibitions I managed to share experiences with many media officials

Key Challenges faced
Technical problems-GPRS, Virus threats, World space receiver
Lack of internet service at Maarifa centre
Lack of adequate information to provide information sought by visitors including books, newspapers, entertainment magazines, and agriculture information.
Inadequate facilities like stationery, computer and cartridge
Transport problem , hindered me to reach remote areas .
6. Lack of fund to manage a Radio Programme



Overcoming the challenges
I frequently traveled to NAFRAC in order to surf information particularly OKN information also to send the created articles.
Providing the few available information to needy people.
Hire bicycle
Lobbying other stakeholder to support a radio programe but not sustainable.
Achievements
§ People became more informed and convinced about ALIN.
§ Different Programmes conducted at NAFRAC were documented and disseminated duly through study visits( political leaders, farmers, extension officers , decision makers), school field excursions etc
§ Publicized NAFRAC and ALIN at Maarifa Centre during Mazingira day exhibitions, this exhibitions was attended by more one thousands peoples and the vice president was a guest of honour also the Minister of Environment Batilda Buriani attended.
§ Publicized Maarifa Centre three(3 ) times through Radio Program Radio Faraja and 6 Program on Radio Sibuka at Maswa.
§ 30 persons from MECHASO were informed on how ALIN work when visited NAFRAC .
§ 4 video Program were produced which include mazingira day .
§ Built good relationship with a Shinyanga Press club thus it is easier for me to get information because their leader always furnishes me with update news conducted at this area .

§ Built network with SNV; Cooperate with SNV to support a health training programmed based on five basic principles of health involving 8 primary schools in Maswa district. The out come of this train now the behavior of student changed when did we visit this school had a healthily club which act like a media person on educating each other on how to protect them selves. 120.student were mobilized and currently use a instrument called Kibuyu chirizi (Swahili) instead of using sink or tape water because many schools in Tanzania particularly in remote areas usually face water scarcity

§ Produced several documents like NAFRAC newsletter, Maarifa newsletter, TAFORI brochure, Maarifa brochure etc
§ Creation of articles from the focal groups that explores the indigenous knowledge.
§ Fund rising from SNV to conduct a Programme called Child to child

Testimonies from users
Through verbal testimonies like; Centre manager and NAFRAC staff members verbally appreciated of the initiatives undertaken by a newly recruited volunteer ‘’Mwantumu’’, That’s me! Because within a short period of time I have been able to produce several documents like NAFRAC newsletter, Maarifa newsletter, TAFORI brochure etc
Readily availability of educative information provided by CKC to the targeted audience
Mr A A chuwa an Agricultural officer had the following to say; “Stakeholders of CKC should be committed and well coordinated, as such a journalist with a strong vision like you is vital for the success of such initiatives”.
Also from the
Also in the CKS there is a suggestion books thre is a aseveral recommendations and appreciation on my work and how to survive.

Lessons learnt
From the testimonies from users and the interest generated by the CKC, this shows that with improved capacity, it can enhance information access and increase awareness to the local community.
The focal group meeting was an eye opener judging from the gender balance achieved and participation by women. The focal group can therefore increase women’s participation in development especially among the Sukuma people.

Monday, December 29, 2008

SALADI YA UKWAJU

VIPIMOKabeji 1/2Karoti 2 Tango
NAMNA YA KUTAYARISHA1.Kata kabeji nyembamba sana2. Zikune karoti zitoke nyembamba3. Kata tango vipande vidogo vidogo.3.Kisha changanya pamoja tia kwenye bakuliUKWAJUVIPIMOUkwaju 1 paketi moja (gm 100)Maji 2 vikombe Thomu chembe tatuTangawizi kipande kidogo tuTende 3 Kitunguu maji 1 kidogoNyanya 1 ndogoPili pili mbichi 3NAMNA YA KUTAYARISHA1.Toa kokwa katika ukwaju 2.lowanisha na maji kisha kamua na utupe kokwa 3. Tia katika sufuria na tia vitu vyote vingine ndani ya sufuria.4.Chemsha, na ikianza kuchemka ipike kwa muda wa dakika 5.5.Epua na uache upoe kisha usage katika mashine ya kusagia (blender) – uko tayari kuliwa na kuku na saladi.

Biringani Za Ukwaju

Biringani Za Ukwaju
VIPIMO
Bilingani 2 Makubwa
Vitunguu maji 2 vya kiasi
Nyanya 2 za kiasi
Thomu uliyosagwa au kuparuzwa 1 ½ Kijiko cha chai
Pilipili mbichi iliyosagwa
(au kukatwa ndogondogo) 1 kijiko cha chai
Chumvi kiasi
Mafuta 2 vijiko vya supu
Ukwaju 1 Kikombe cha chai
Vitunguu vya kijani (spring onions) mche mmoja
Mafuta ya kukaangia mabilingani

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Kata mabilingani nusu kwanza, kisha kata vipande kwa urefu vya kiasi 1.5 cm
2. Kaanga mabilingani katika mafuta ya moto kabisa, mpaka yageuke rangi. Epua na yaweke katika chujio yachuje mafuta.
3. Kataka vitunguu vidogo vidogo (chopped), kaanga mpaka viwe vyekundu kidogo.
4. Tia Thomu kaanga kidogo tu.
5. Tia nyanya zilizokatwa ndogo ndogo (chopped) endelea kukaanga mpaka ziwe laini, ukiongeza pilipili mbichi iliyosagwa na chumvi.
6. Yapange mabilingani katika sahani au bakuli la kupakulia na mwaga rojo ulilokaanga juu yake.
7. Mwagia ukwaju na changanya vizuri kwa pole pole yasivurugike mabilingani.
8. Pambia kwa vitunguu vya kijani (spring onions) viliyokatwa vidogo vidogo (chopped) – Tayari kuliwa.

Kidokezo:
Ni nzuri sana kuliwa na mikate mikavu kama mkate wa ufuta au Naan au mkate wa Ki-Lebanon (Pita Pain)

Mchanganyiko Wa Mboga Za Kuchoma (Baked)

Wakulima wamekuwa wakivuna mboga nyingi katika mashamba yao na kutafuta ni njia ipi itumike kuhifadhia mboga mboga na matunda ambazo ndio lishe bora kwa familia zao .Bi Zakhia Swai mwenye umri wa miaka thelathini na tatu anatufundisha katika eneo la Boma ng'ombe wanavyohifadhi mchanganyiko wa mboga mbalimbali.

Vipimo

Viazi 5

Karoti 2

Koliflawa (cauliflower) ½

Brokoli 3 misongo (bunch)

Pilipili mboga ya kijani 1

Pilipili mboga nyekundu 1

Thomu iliyosagwa 1 kijiko cha supu

Pilipili manga iliyosagwa 1 kijiko cha chai

*Kidonge cha supu (stock) 1

Parsley kavu iliyokatwa ndogo ndogo (chopped) 2 vijiko vya supu

Chumvi kiasi

Mafuta ya zaytuni (olive oil) 3 vijiko vya supu


Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Menya viazi katakata vipande vya mchemraba (cubes)
Katakata karoti vipande virefu virefu vya kiasi
Katakata mapilipili mboga vipande vya kiasi kiasi
Chambua koliflawa na brokoli
Tia mafuta katika karai, kaanga thomu kidogo kisha tia chumvi, pilipili manga, epua weka kando.
Weka kidonge cha supu katika kibakuli kidogo, tia maji ya moto kiasi vijiko 3 vya supu, koroga kipate kuyayuka iwe supu. Tia katika sufuria uliyokaangakia thomu.
Weka mboga zote katika bakuli kisha mimina mchanganyiko wa thomu na supu uchanganye vizuri.
Tia katika treya ya kupikia ndani ya oveni. Zipike mboga (bake) kwa moto wa takriban 350°C kwa muda wa dakika 15-20.
Epua kisha mwagia parsely na uchanganye kisha mimina katika bakuli la kupakulia ikiwa tayari kuliwa kwa aina za mikate.
kidonge cha supu ikiwa ni chicken stock au beef stock.

HABARI NJEM A KWA WAFUGAJI?

HABARI NJEM A KWA WAFUGAJI?
Na.Mwantumu Jongo.
Suala la matumizi ya madume bora ya ng’ombe ni kitu cha lazima kwa wafugaji wa ng’ombe wa asili, kama wanahitaji kujinasua katika umasikini. Wafugaji wa ng’ombe wa asili, wanatakiwa kuboresha mifugo yao ili iweze kufikia viwango vya kimataifa. Viwango hivyo ni pamoja na kuwa na umbo la kuridhisha na uzito mkubwa, ukilinganishwa na ng’ombe wa sasa wenye maumbo madogo na uzito usiokidhi soko hilo la kimataifa. Kituo cha Taifa cha Madume Bora ya Mbegu za Ng’ombe (NAIC) cha Usa River, Arusha, kina jumla ya madume 25 kwa sasa. Madume hayo ni kwa ajili ya kuzalisha mbegu bora za ng’ombe wa maziwa na nyama. Wizara ya Maendeleo ya Mifugo, imeanza kuchukua hatua kadhaa ili kuwakomboa wafugaji wa ng’ombe wa asili katika ushindani wa soko la kimataifa. Moja ya hatua hizo ni kutoa huduma ya mbegu bora za madume, ambayo itaweza kuwatoa katika aina duni ya ng’ombe wanaomiliki hivi sasa. Hivi karibuni nilitembelea kituo hicho cha madume bora. Kituo hicho hakifahamiki sana na wafugaji wa ng’ombe wa asili. Wafugaji wengi niliowahoji walisema hawatambui kuwapo kwa kituo hicho muhimu kwao katika kufanya mageuzi ya kibiashara hatua kwa hatua. Wachache walisema wanadhani kituo hicho kinajishughulisha na uzalishaji wa mbegu bora, kwa ajili ya ng’ombe bora wa maziwa. Kwa kifupi, Kituo cha Mbegu Bora cha Taifa (NAIC) kina ukubwa wa eka 315, ambapo eka 45 kati ya hizo, zinamilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Arumeru, kwa ajili ya upanuzi wa mji wa Usa River. Eka 50 ni msitu wa asili, eka 40 ni majengo, eka 53 ni eneo la maabara, eka 27 ni miamba na eka 135 ni maeneo ya kulima majani kwa ajili ya madume yanayofugwa hapo. Kituo kina uwezo wa kutunza madume 88 na mahitaji ya malisho ni eka 2.5 kwa dume moja. Hivyo madume 88 yanahitaji eka 170. Madhumuni ya kuanzisha kituo hicho ni kuongeza uzalishaji wa maziwa na nyama ili kuinua pato la Taifa na la wafugaji na kuboresha lishe nchini. Kuzalisha mifugo kwa njia ya uhamilishaji, kunasaidia kuzuia gharama zisizo za lazima, kutunza madume na kuepukana na hatari ya kujeruhiwa na madume au dume kujeruhi ng’ombe wenzake. Njia hii pia inasaidia kuzuia kuenea kwa magonjwa ya vizazi na kusafirisha mbegu bora kirahisi kutoka eneo moja hadi jingine. Njia ya uhamilishaji pia inafanya mfugaji apate ndama wengi, kutokana na dume moja kwa muda mfupi kwa sababu dozi 200 na zaidi za mbegu, zinaweza kukusanywa kwa siku moja kutoka kwenye dume moja. Kwa njia ya asili dume moja hupanda majike 30 kwa mwaka. Mbegu za dume zinaweza kuvunwa leo na kukaa muda mrefu, hata kama dume huyo atakuwa amevunjika au kufa, kwa sababu mbegu zake zinahifadhiwa na kutunzwa kwa muda wa miaka 20 na zaidi zikiwa hai. Vile vile inasaidia mfugaji kuwa na wigo mpana kuchagua aina ya mbegu anayohitaji. Pamoja na kuzalisha mbegu bora za madume, NAIC kinazalisha hewa baridi ya nitrojeni, kwa ajili ya kuhifadhia mbegu. Bila hewa hiyo huwezi kuhifadhi mbegu hizo, hii ni pamoja na kutoa vifaa vya uhamilishaji, ambavyo ni mitungi ya kuhifadhia na kusafirisha mbegu, bunduki na mirija ya kupandishia ngombe na glovu za kuvaa mikononi. Pia NAIC kinafundisha wataalamu wa uhamilishaji, ikiwa ni pamoja na watu binafsi na wataalamu wanaoteuliwa na vikundi vya wafugaji. Vile vile hutoa mafunzo na taarifa muhimu kuhusu ufugaji kwa vikundi vya wafugaji na wakulima, kutunza kumbukumbu za uhamilishaji, kupima mimba changa kwa kutumia maziwa. Kwa sasa kituo kina madume 25 ya aina za Ayrshire madume tisa Fresian, madume matano Jersey. Aina hizo tatu za madume ni kwa ajili ya maziwa. Aina nyingine ya madume matano ya Sahiwal na madume manne aina ya Mpwapwa. Aina hizo mbili za madume ni kwa ajili ya maziwa na nyama. Aina ya mwisho ya madume ni madume aina ya Boran, ambayo yapo matatu. Aina hii ni kwa ajili ya nyama. Kwa sasa sehemu kubwa ya mbegu za ng’ombe wa nyama, zinatumika kwenye mashamba ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO). Hivyo basi, wafugaji wa asili wanaofuga karibu na ranchi za taifa wanayo nafasi kubwa ya kujiweka katika vikundi na kuomba kupata elimu na gharama za uhamilishaji kutoka katika ranchi. Hii itakuwa ni nafasi nzuri kwao kuanza kupata huduma ya uhamilishaji na kubadilisha ubora wa uzao utakaozaliwa kwenye mifugo yao. Madume aina ya Sahiwal ni mazuri kuhamilisha kwa ng’ombe wa asili ili kuweza kupata ng’ombe wenye nyama nyingi watakaokidhi soko la nje. Dume aina ya Sahiwal ni maarufu kwa ajili ya nyama na maziwa. Dume huyo ana kawaida ya kuzaa watoto wenye sifa ya kutoa maziwa na ukuaji wa haraka. Asili ya dume huyo ni Nakuru, Kenya. Aina hiyo ya ng’ombe inafaa sana kwa wafugaji wa mikoa ya Shinyanga, Arusha na Dodoma. Wanahimili magonjwa na ukame, wanakua haraka sana na wana umbo kubwa lenye nyama. Dume aina ya Boran anaongeza nyama kwa ng’ombe wa asili. Wafugaji nchini wanaweza kutumia aina hiyo ya madume katika shughuli zao za ufugaji, kutokana na ukweli kwamba aina hiyo ya madume huwezesha kupatikana aina nzuri ya ng’ombe wa nyama na maziwa. Hatua hiyo inaweza kuwasaidia kujiongezea pato lao na la Taifa kwa ujumla.