Tuesday, February 10, 2009

CHANJO YA PEPOPUNDA KWA WANAWAKE

Na.Mwantumu Jongo
Pepopunda ni ugonjwa wa hatari unaoambukiza na bacteria ambao huingia mwilini kupitia kwenye kidonda au jeraha .Ugonjwa huu huwapata watu wa rika zote .chanjo ya pepopunda kwa wanawake kila mwanamke kuanzia umri wa miaka kumi na tano na arobaini na nne ni muhimu akamilishe chanjo dhidi ya pepopunda .

Katika sehemu nyingi duniani wanawake hujifungua katika mazingira machafu hii inamuweka mama na mtoto katika hali ya kupata ugonjwa wa pepopunda ambao huuua watoto wachanga wengi kama mama hakupata chanjo ya pepopunda mtoto azaliwaye ni rahisi kuupata ugonjwa huu.

Vijidudu vya ugonjwa wa pepopunda huzaliana kwenye majiraha machafu hii inaweza kutokea ikiwa kiwembe kisu kichafu kitatumika kukatia kitovu cha mtoto au kitu chochote kichafu kikiwekwa kwenye kitovu cha mtoto mchanga .kitu chochote kinachotumika kukatia kitovu cha mtoto ni sharti kwanza kioshwe au kiunguzwe kwenye moto na baadae kuachwa kipoe.

Wanawake wote wanaofikia umri wa kuzaa wapate chanjo dhidi ya pepopunda wanawake wajawazito wahakikishe kuwa wamepata chanjo hizo na kwa namna hiyo mama na mtoto atakayemzaa atakuwa amepata kinga dhidi ya ugonjwa huu.kama mamajamzito hajawahi kuchanjwa apewe chanjo ya pepopunda mara moja chanjo ya pili itolewe wiki nne baadae chanjo ya tatu miezi sita baadaya chanjo ya pili chanjo ya nne nay a tano zitolewe mwaka mmoja baada ya ile iliyotangulia ikiwa mwanamke amepata chanjo ya ugonjwa huu maratano atakuwa amepata kinga dhidi ya ugonjwa huu katika umri wake wote wa kuweza kuzaa .na mtoto atakuwa amekingwa na ugonjwa wa Pepopunda.
Shime wakinamama hakikisheni mnapatiwa chanjo hii kwa usahihi na serikali iwe mstari wa mbele katika kusogeza huduma hii karibu na wananchi ili kupunguza idadi ya vifo vya kinamama na watoto.

HATUA ZA VVU KATIKA MWILI WA BINADAMU

na.Mwantumu Jongo
Katika mwili wa binadamu ni muhimu sana kwa kila mmoja wetu kupima damu kujua kama unaishi na Virusi vya UKIMWI(VVU) au la kuna hatua tatu tofauti za VVU.

UNA VVU UNA AFYA NZURI.
Katika hatua hii inamaanisha kuwa mfumo wako wa kinga mwilini uko imara na idadi ya CD4 zako ziko juu huhitaji kutumia dawa za kupunguza makali ya vvu (ARV)kama ni mzazi waandae watoto wako kwa kuwaeleza kuhusu VVU .Hakikisha wataangaliwa vizuri pindi utakapozidiwa na ugonjwa au utakapofariki .Tafuta msaada wa kukusaidia kukabilia
na na hali hii.

UNA VVU NA UMEZIDIWA NA UKIMWI
katika hatua hiii unagua sana mara kwa mara hupati nafuu .Inamaanisha kwamba mfumo wako wa kinga ndio dhaifu sana lazima upate matibabu kwa magonjwa yako ambayo hushambulia mwili wakati kinga imepungua huitwa magonjwa nyemelezi shauriana na muhudumu wa afya kuhusu kuanza kutumia ARV. Kwa kawaida watu hufuata matibabu wakati wakiwa wagonjwa na hawajiwezi na kama unatunza mgonjwa na anatumia ARV hakikisha unaelewa vizuri kuhusu dawa hizo zungumza na muhudu wa afya kwa maelezio zaidi .

UNA VVU NA UNAANZA KUUMWA
Katika hatua hii mfumo wako wa kinga unaanza kuwa dhaifu muombe muhudumu wa afya akupime idadi ya CD4 kwenye damu yako .Hii itakuwezesha kufahamu kuanza kutumia ARV .Magonjwa unayoyapata unapokuwa na VVU yanaweza kutibika lakini lazima uwe mwangalifu kwa sababu baadhi ni magonjwa hatari ni muhimu kwenda hospitali hospitali.

MAONI
Mgonjwa ahakikishe akishajua kama ameathirika na Virusi vya UKIMWI ahakikishe anapata ushauri nasaha na kuwahi kutumia dawa za ARV kwani kwa kufanya hivyo kutamsaidia mgonjw ahuyo kuongeza muda wake wa kuishi .

Tuesday, December 30, 2008

CHILDREN TO CHIDREN CLUB.

Na.Mwantumu Jongo.
This is a health club which established for the aims of educating the student about health in the primary level. C to C it is a combinations of students and health’s teachers with the aims to educate about health’s in their schools.

In the early in Shinyanga region there is a problem of the student did not know five basic s of health and it’s a main source of environment pollution.Maarifa resource in cooperation with Radio Sibuka and SNV discover this problem it’s a main source and a take a time and discuss we realise that a children used a many time at school so when educated about health issue through CtoC club because we believe a children had a power to educate the society it is easy to them to protect his /her health and when this children retuned home he or she can at as a good advisers on their families for this perception this C to C club stimulate the development.

A children on C to C club had a capacity to educate society through a songs, comedy, drama and drawing an example when the children see the person goes inverse on the health basics he/she can sing a song with the aim to educate health theme so that person he/she know that’s action it is not good in the society .

Tools&Techniques
Supported Telephone to 8 Primary school at Maswa District which conducted a C to C club.
To express the project at the administration level which include the district commissioner and Regional commissioner?
To build a capacity building to the radio representer, health teachers and student on how to run a c to c club and its duties and obligation .The c to c club was taught 5 basic health on health of environment and personal health, reproduction health, availability of pure water and safety, Immunization against diseases.

RESOUCES
§ Human resources he/she can mobilize the teachers & student to initiated a C to C club in their schools .
§ Fund to manage a Radio Program and facilitator.
§ Telephone and radio inoder a C to C club to listen a live programme and participate fully to share their vies and ideas .


Lesson learned
To have a frequently radio program and money to run this C to C club operation. My suggestion is that insure you have enough money when invest this project at your place and leave the student be free to find out a way to educate the society. Monitoring must be regularly and at a specific time.

Now the student habit changed due to know health basic many school at Tanzania hasn’t a dust bin normally use a hole so it is very difficulty for the newcomer or a guest to keep the environment safety these club hang viroba( plastic bag) at each tree surround school environment when he/she use a solid waste put on the plastic bag in Kiswahili so the school compound was so clean.

Smartness of the student increased due to know personal cleanness her is no wastage of time for a teacher to punish the dirty student because the student educated them selves each an example a student ask other student don’t you know the dirty is not a good habit can cause to you a disease and perhaps the student academic rise d because the student had not get a punishment from the teacher and the student love that teacher .

STRATEGIES
§ To find a radio sponsor inoder the radio Program to be runned at the three months before the contract end to rise awareness.
§ To have a good radio presenter inoder to communicate well with a C to C club to express and share information .
§ To conduct a training on a C to C club to build a capacity for C to C club to be knowledge on how to educate the society.

ADAPT AND APPLY BEST PRACICE
§ First of all introduce the theme or project to the Administration level these include reginal commissioner.
§ Capacity building to the students ,teachers and radio presenter.
§ The student must plan and take ana actions.




AN EXAMPLE OF DUTIES & OBLIGATIONS ON THE HEALTH CLUB

RESPONSIBLE PERSON
DUTIES
TEACHERS
To organise a health club on their school.
To taught a student a how to express their view to the society and how to educate the society through asongs and comedy.
STUDENT
To plan and to do an actions like how to protect their environment through organising public sanitation , how to get ana excess on pure water and implement their plans .
REPRESENTER
To insure that the radio programme sustanablility.

§ Arrange the live Radio Program and the student express their view to the public.
§ Monitoring and revaluation through the study visity the student can move from one school to another to learn what other practice.

MKOJO WA KONDOO HUHIFADHI MBEGU ZA MAHINDI

Na.Mwantumu Jongo.
Mbegu za mahindi huhifadhiwa ili zisiharibiwe na wadudu kwa kumwagiwa mkojo wa kondoo .Kuna njia nyingi za kuhifadhi mazao yetu lakini wasukuma wamenitolea kali ya mwaka kwani wao wanahifadhi mbegu zao za mahindi kwa namna ya pekee tumezoea kuona mbegu hii zikihifadhiwa kwa kufungwa mahindi pamoja na majani yake na kuhifadhiwa juu ya dali la jiko ili ziweze kukaushwa na moshi wa jikoni.

Lakini katika eneo la Kitangili lililopo karibu na stesheni ya reli mjini shinyanga ndipo nilipokutana na uvumbuzi wa aina yake kwani bwana Kulwa Steven alisema tangu utoto wao huhifadhi mbegu za mahindi kwa kutumia njia hii .

Ambapo mkulima hutayarisha “jeka”ni sehemu ya kuhifadhia mbegu kama vile ilivyo mtungi .Kuna njia mbili za kujenga jeka,mahitaji yake ni kamba ,miti mirefu na mifupi na mabua.Katika njia ya kwanza mkulima hutafuta miti mirefu , na nguzo fupi anachimbia chini ya ardhi ,kisha analaza fito mstari mmoja halafu zile mbegu za mahindi anazifunga kwa kuyaunganisha majani ya yale mahindi yenyewe kwa yenyewe na kuanza kuyapanga kwenye fito njia hii kwa kisukuma huitwa nshijite .

Njia ya pili ni ile Mkulima hutafuta miti mirefu na mifupi anatengeneza kichanja halafu pembeni anasimamisha miti mirefu halafu anasiliba na mabua unaweza ukatengeneza kajumba kwa juu ili kuzikinga mbegu zako katika kipindi cha kiangazi .

Mkulima huchukua mahindi mabichi hayatoi majani yake unayaunganisha na kuyafunga pamoja kisha unayahifadhi kwenye jeka lake .Vijana hutumwa kuleta mkojo wa kondoo ambao hupatikana kwa kumshika kondoo na mwengine hukinga ule mkojo inasemekana kondoo ni nadra kukojoa lakini akishikwa hukojoa haraka na kumwagia katika jeka lenye mbegu za mahindi .Mbegu za mahindi huweza kuhifadhiwa kwa njia hii kwa muda wa mwaka mmoja na zaidi bila kuharibiwa na wadudu.

Bwana Steven anaamini wadudu hawapendi harufu ya mikojo ya kondoo hivyo wakikaribia katika jeka huondoka mara moja na kuziweka mbegu zao katika hali ya usalama .
Kwa upande wangu nimebahatika kuona njia nyingi za kuhifadhi mbegu za mahindi kama vile kuhifadhi katika mti wenye njia panda unalaza mti na kuyafunga mahindi yako nji hii na nyinginezo hutumika sana katika vijiji vingi nchini Tanzania hivyo hatuna budi kuzitumia ili tuweze kuwa na uhakika wa kuhifadhi mbegu za mahindi.
Serikali na taasisi binafsi ziziendeleze njia hizi za asili kwa kufanyia utafiti ili kuwa na uhakika zaidi wa ubora wa njia hizi kwani tukumbuke kuna usemi usemao kuwa ya kale ni dhahabu.

KILIMO MSETO NA MAENDELEO YA JAMII

Na.Mwantumu Jongo.
Kilimo mseto ni elimu iliyomuwezesha Ndugu Joseph Seni na wakulima wengine kupata maendeleo ya haraka .Katika nchi yetu kilimo mseto ni moja ya kilimo kilichokuwa kikifanywa na babu zetu ingawaje hawakutambua kama walikuwa wakifanya kilimo hiki wazee wa zamani walikuwa wakiachia aina fulani ya miti mashambani ili kupata kivuli kama sehemu ya kupunzikia shambani ,wakiachia miti ya matunda na miti mingine ya dawa mashambani ,miti iliyokuwa ikiachwa ni miti ambayo ilikuwa haidhuru mazao na inapukutisha majani yenye kuongeza rutuba ardhini ,pia walikuwa wakihifadhi eneo Fulani la malisho kwa ajili ya ndama na ng’ombe wagonjwa hii yote ilikuwa ni namna ya kilimo mseto.
Baada ya uharibifu mkubwa wa mazingira kuanza kutokea wataalamu waliamua kuboresha kilimo asilia na kupata kilimo kijulikanacho kama kilimo mseto elimu ambayo kwa sasa inahitajika sana ili kunusuru hali ya uharibifu wa mazingira duniani.
Mchungaji Joseph Seni ni mkazi wa kijiji cha Mwasele Lubaga tangu mwaka 1994 alianza na shamba la kilimo lenye ekari mbili na kutokana na mafanikio ameweza kununua shamba jingine hadi kufikia hekari nne(4).Bwana mstaafu wa kanisa la (PEFA)pentecoste Evangelistic Fellowship Africa Shinyanga ,alistaafu kazi ya uchungaji na kujiunga kitengo cha uinjilisti uenezi mwaka 1994 na baada ya kustaafu uchungaji bwana Joseph Seni aliweza kuanzisha kilimo mseto kwa kutekeleza baadhi ya vifungu vya Biblia vinavyohusu utunzaji wa mazingira .
Mchungaji huyo ni miongoni mwa wakulima waliopata mafanikio makubwa baada ya kupata elimu ya kilimo mseto baada ya kuona mafanikio yake mchungaji amejitolea kuelimisha jamii kuhusu kilimo hiki na manufaa yake kwa kuanzisha vikundi vya kilimo mseto na ngitili ,utayarishaji na uhifadhi wa malisho kwa njia bora.Biblia kwa kutumia maandiko matakatifukutoka katika kitabu cha mwanzo 2:8na mwanzo 2:15 mchungajiamefanikiwa kushawishi watu wengi kuanzisha shughuli za utunzaji wa mazingira .

Mwanzo 2:8 inaeleza yafuatayo ;
‘Bwana mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni akamweka ndani yake mwanandamu .
Mmwanzo 2:15
Bwana mungu akamtwaa huyo mtu akamweka katika bustani ya Edeni ailime na kuitunza’kwa kutumia maandiko matakatifu yaliyotajwa ni kwamba yanaikumbusha jamii ya kuwa dunia iliumbwa na kuwekewa mazingira mazuri ila kwa matumizi ya mwanandamu ndiye aliyeanza kuyaharibu mazingira yake hivyo inatupasa tuyatunze kama mungu alivyotuamuru ni dhahiri kwamba bwana aliweza kueleweka vizuri .
Siri ya mafanikio ya mchungaji ni kwamba pamoja ya kusoma maandiko matakatifu ndani ya biblia aliweza pia kujisomea kitabu chake kiitwacho ‘Mkulima stadi(P.Otma Monger OSB na P.B Ngeze NdandaPublication 1941,1985)ambacho kinaelezea fani mbalimbali za kilimo na ufugaji aliwahi kukutana na mkulima mmoja bwanan Antony Katakwa ambaye tayari ameshaanza kilimo mseto kwa msaada wa Shinyanga Mazingira Fund.
MAFANIKIO
Ndugu Joseph amefanikiwa kusambaza elimu hii kwa watu wengi ikiwa ni pamoja na kikundi cha Juhudi na maarifa group na makundi ya kikristo mfano mzuri Mwamagunguli,Iselamagazi PAG ,Mongolo Kahama PEFA,Muhina Mwamapalala Maswa .
Kuanzisha bustani za miti Iselamagazi,mwamagunguli,Kitangiri na Chibe.
Alianza na ufugaji wa kuku wakaongezeka hatimaye kubadilishana kupata mbuzi na hatimaye kupata n’gombe .Ameweza kuongeza shamba kutoka ekari 2 hadi 4 kwa sasa .Ameongeza mavuno katika shamba lake kutoka gunia moja(1) hadi kumi na sita(16)za mahindi kwa ekari tatu .
Ameweza kuanzisha shamba la malisho yanayotosheleza mifugo yake na ziada anauza na kupata kipato .
Ameweza kuanzisha ufugaji nyuki .Ameboresha maisha yake na kutengeneza nyumba bora ya bati.
MATARAJIO YAKE
Anatarajia kubadilisha mifugo ili apate ng’ombe wa maziwa ,kuanzisha bustani ya matunda ,kuanzisha bustani ya kuzalisha uyoga.
Pia anatarajia kutoa elimu kwa vijanailia wapate kujiajiri kupitia rasilimali zinazopatikana kwa kutunza mazingira.
USHAURI
Kutokana na tafiti mbalimbali za kilimo mseto zimeonyesha kuwa jamii inaweza kufaidika sana kwa kulima kilimo hiki kwani kilimo mseto kimeshafanyiwa utafiti kwenye makundi makuu manne ambayo yanamsaidia mkulima ,mfugaji mifugo,mfugaji wa nyuki na mfugaji wa samaki kwenye eneo dogo kupata kipato kiubwa .
Ni vizuri tuige mfano wa mchungaji Josepaliyeweza kutumia eneo dogo la kilimo na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kutoka katika eneo moja.

UVUNAJI WA MAJI KWA NJIA YA MAJALUBA

Na.Mwantumu Jongo.
Kitangili ni eneo linalopatikana katika wilaya ya Shinyanga mjini baadhi ya wakazi wake wanalima mpunga kwa kutumia mitaro badala ya maji ya mvua kumwagika ovyo yanaelekewa kwenye mashamba maarufu kama majaluba.Majaluba ni sehemu iliyoandaliwa kwa ajili ya kupanda mpunga.Njia hii husaidia sana katika kuhifadhi maji hususani katika maeneo ya nyanda kame ili kuweza kuongeza uzalishaji katika eneo dogo.

Upatikanaji wa maji katika majaruba unafanyika kwa kutengeneza mitaro inayotiririsha maji na kuielekeza kwenye majaruba. Utengenezaji mitaro unahitaji ushirikiano hasa pale kunapokuwa na majaruba mengi yanayomilikiwa na wakulima mbalimbali.

Hivyo mitaro hii hutengenezwa na wakulima kwa kuyaelekeza maji ya mvua katika majaruba yao. Njia hii imekuwa na manufaa sana kwani hakuna maji yanayoachwa ovyo. Kwa hiyo hii ni namna mojawapo ya utumiaji mzuri wa maji.

Hali hii imewafanya wakulima wengi kupanua mavuno yao. Awali mkulima alingoja mvua tu huku miteremko ya maji ikitiririsha maji ovyo. Baada ya ugunduzi huu wa taaluma hii, wakulima wamejikuta wakinufaika sana. Sasa hivi wakulima wamenzisha vikundi vya kutengeneza mitaro ya namna hii katika azma ya kuboresha kilimo cha mpunga.


UTAYASHAJI WA JARUBA
Unalima na kuweka kingo nne za matuta baada ya siku saba unayachanganya majani yaliooza na udongo ni mbolea. Majani yasiyooza unayalundika pembeni ya shamba ili yasiote huchanganywa na udongo baada ya mavuno hutumika kama mbolea. Unaangalia uelekeo wa maji ardhi iwe sawa ukiona kilima unashushia kwenye bonde hii inasaidia kutunza maji kwani mpunga unahitaji maji mengi.Hakikisha miche ya mpunga haizami kwenye maji .

KUOTESHA MBEGU
Kipindi cha mwezi wa kumi mkulima huotesha mbegu kwa ajili ya kilimo cha mpunga kuna njia mbili za kuotesha mbegu njia ya kwanza ni ile ya kulima kitalu pembeni ya jaluba sehemu yenye unyevu nyevu na kuotesha mbegu zikiota miche ikikuwa ndipo huhamishwa na kupanda kwenye majaluba yaliyoandaliwa .
Aina ya pili ni kutifua jaluba na unamwaga mbegu za mpunga ndani ya jaluba zima kwa kusubiri mvua ili mbegu iote.

UPANDAJI
Miche ikikuwa unangoa na kupanda katika jaluba katika njia ya pili kama imeota miche imeota mingi unahamisha na kupanda katika jaluba jingine eneo likiwa na rutuba nyingi unapanda mche mmoja.Majaluba yan milango ya kupokea maji na kutoa mfano mpunga ukianza kucahnua unahitaji maji hivyo milango yake huwa wazi ili kuingiza maji kwenye jaluba.
UPALILIAJI
Kwenye jaluba kukiwa na maji ya kutosha majani yanakufa kwa kuoza katika maji ardhi inakuwa laini mkulima huyangoa na mkono lakini unatakiwa uchukue tahadhari kwani majani ya mpunga yanafanana na magugu hivyo unashauriwa usubiri hadi miche ifikie inchi kumu na tano(15).
UVUNAJI
Baada ya takriban miezi mitatu, uvunaji wa mpunga huanza. Uvunaji uko katika njia mbili nazo ni (a) uvunaji wa kutumia kisu kwa kukata kila kikonyo cha mpunga (b) uvunaji wa kutumia kiberenge yaani kukata shina lote la mpunga kwa kukusanya katika makundi makundi.
Kisha unaandaa sehemu safi ambayo itakuwa haina mchanga. Eneo hili utatumia jembe kuondoa nyasi na mchanga. Fagia eneo lako kwa kuondoa mchanga. Pale inapobidi, unaweza kutumia mavi mabichi ya ng’ombe kwa kuyafanya yawe mazito kiasi. Changanya katika ndoo hakikisha hakuna mabonge mabonge ya mavi ya ng’ombe.
Chukua mfagio mgumu wa nje na kumwaga huo mkorogo wa mavi ya ng’ombe. Fagia mkrogo huo na kuacha mwingine unate sehemu uliyoandaa. Ukisha kamilisha acha pakauke. Unaweza ukapaacha pakauke kwa muda wa masaa mawili au matatu na kuanza kazi.
Somba mpunga wote uliokata na kuurundika katika eneo uliloandaa kwa ajili ya kupigia. Daima unapoleta panga katika mstari katika duara kwa kurundika ukiacha nafasi kigodo katikati. Anza kuchukua kiasi unachoweza kukiwebeba mikononi na kukiinua juu kisha kipigize sehemu uliyoacha wazi. Pigiza mara tatu au nne kutegemea hakuna mpunga unaosali kwenye majani ya mpunga. Endelea hadi rundo lako limekwisha.

Kama kuna mpunga mwingine, endelea kufanya hivi mpaka umalize. Ukiona umechoka, unaweza kuamua kupeta mpunga uliopiga kwa kutumia ndoo. Chota mpunga kadri unavyoweza kubeba na kuinua juu pembeni kidogo mwa mpunga uliopiga. Mwaga kidogo kidogo utaona pumba na uchafu mwingine unapeperushwa na upepo.na hivyo mpunga safi kubaki karibu na miguu yako. Endelea mpaka umalize rundo la mpunga uliopiga.
Kazi itakayofuata ni kuweka katika mifuko unashona na kusafirisha nyumbani.Kazi ya uvunaji itakuwa imekamilika.
Uvunaji wa kukata kila kikonyo cha mpunga unafanyika kwa uchache sana kwani unapoteza wakati mno na pia nguvu nyingi. Mpunga unapokuwa umevunwa, huwekwa ndani kwa muda wa mwezi mmoja au miezi miwili ili ukauke vilivyo. Hatimaye eneo maalum la kupigia kama nililolieleza hapo juu huandaliwa. Mpunga hutolewa nje na kuachwa kwa muda mfupi ukauke. Kazi inayofuata ni kupiga mpunga kwa kutumia fimbo ndogo ndogo. Upigaji huu ni wa kuhakikisha kuwa hakuna mpunga unasalia kwenye vikonyo vyote.
Kazi ya kupeta inafuata baada ya kumaliza kupiga. Baada ya kupeta mpunga hujazwa katika magunia ama huwekwa katika ghala.

MAFANIKIO
Mavuno mengi katika eneo dogo.
Shamba kuwa na rutuba
Kukiwa na maji ya kutosha kama kukiingiliana na mto kuna uwezekano mkubwa wa kupata samaki.

MATATIZO
Wadudu waitwao ngegeshi hupatikana wakati maji yakiwa yamepungua hukata majani ya mpunga.
Ndege ambao kwa sasa hutumia njia za kienyeji kuwa fukuza kama kuchonga masanamu yanayofananna na watu,kanda za redio hufungwa pembeni mwa kingona hata mabetri hubondwa na lie bati lake kwa vie tu lina mngao huwakimbiza ndege.

SUNGUSUNGU WATUNZA MAZINGIRA

Na.Mwantumu Jongo.
Wengi wetu tumekuwa tukifahamu kuwa sungusungu ni jina la wadudu wadogo wadogo weusi ambao hutambaa ardhini.Wadudu hawa huuma pindi wanapokandamizwa.Mtu aumwapo na wadudu hawa huisi uchungu. Neno hili lilipendekezwa litumike kwa kikundi hicho cha Usalama kwa sababu ya kujihami kwao kwa haraka wawapo na tatizo.
Licha ya kwamba sungusungu hawa adhabu zao haziendani na sheria ya nchi mfano mzuri aliyetengwa haruhusiwi katika kufanya ibada lakini wana mchango mkubwa katika kutunza mazingira yetu.

“Kutunza mazingira ni sehemu ya kazi yao “alisema bwana W.C.Mlenge.
NAFRAC ilipoanza mradi ilikuta sungusungu imeshatawazwa . Mnamo mwaka 1992 mwezi wa saba walienda Bariadi kufanya utafiti wa taasisi za kiasili zitasaidiaje katika kutunza mazingira wakaitisha mkutano wakiongozwa na chifu wao wa zamani ambaye alijua mambo ya mila na uhusiano mzuri (Mhola)Dagashida waliendesha mkutano vizuri.
Ndipo tulipooona dhahiri kuwa wahenga hawakukosea waliposema tunza mazingira nawe ya kutunze ni usemi uliokuweko toka enzi za mababu zetu sungusungu hawa waliweza kutunza mzingira yao kwa vitendo .
Toka jadi wao ndio walikuwa walinzi wa misitu ya asili hawakuishia hapo walikuwa wanalinda kisima kisichafuliwe kwa kutunza misitu ulio karibu na kisima ili kiwe na maji mengi .
sungusungu walianzisha na kuyatunza maeneo mengine ya kulishia mifugo maarufu kama ngitili hao ndio walikuwa walinzi wakuu mfano mzuri katika vijiji vya Ikonda,Busongo,Mwamishani wanataratibu zao za kutunza ngitili kwa kufanya hivyo waliweza kupunguza kulishia mifugo eneo bila ya ruhusa ya mwenye eneo hilo ukikutwa walikuwa wanakuadhibu kisheria .

Pia waliweza kutatua migogoro ya mipaka ya mashamba katika eneo lao hii ilisaidia katika jamii za kisukuma kuishi kwa amani na upendo .Sungusungu wapo katika kamati za mazingira hivyo hutoa mawazo mazuri katika utunzaji wa misitu ya asili na wao ndio watekelezaji wakuu wa suala zima la utunzaji wa mazingira.
Kuwinda ,kuchunga na kukata miti kulikatazwa kulifanywa kwa ruhusa maalum kutoka kwa mwenyekiti wa sungusungu ukikutwa unalipa faini hii ilisaidia sana jamii ya kisukuma kuweza kuwa na mazingira yaliyoboreshwa kiukamilifu.
Nilikuwa na kiu ya kujua asili hasa ya sungusungu ni nini ndipo hapo bwana mwenyekiti wa sungusungu wa Lubaga aliponielezea sungusungu ilianzishwa mwaka 1982 katika kijiji cha ng’wang’halanga wilayani Nzega. Mzee Mwanamabonde alianzishwa sungusungu baada ya kukutwa na watu walokuwa wameibiwa ng’ombe.
Basi Mwanamabonde akiwa mwenyekiti wa kijiji hicho aliwaambia kuwa pamoja na ng’ombe kuwa wako kwa bwana Pandasahani, itakuwa ni vigumu au haitawezekana ng’ombe hao muwachukue hivi hivi tu.

Mzee Mwanamabonde akawaambia tulieni hapa kwanza. Basi Mwanamabonde akaitisha mkutano wa wanakijiji wake kisha wakaenda pamoja nao kwenye mji wa Pandasahani ambapo ng’ombe mbalimbali wa wizi walitunzwa hapo.

Ilikuwa ni siku Pandasahani alikuwa ameamua kufanya karamu kwani walikuta ng’ombe amechinjwa, nyama zikipikwa jikoni. Jamii iliyochoshwa na vitendo vichafu vya Pandasahani iliwaamuru wake zake Pandasahani kujitwisha vyungu vya nyama kutoka jikoni bila kujali wanaungua kiasi gani. Pandasahani aliambiwa wanapelekwa kituo cha Polisi. Wakiwa pamoja na Pandasahani na familia yote, waliongozwa hadi katikati ya pori ambako waliambiwa kuwa hapa ndiyo kituo cha Polisi.

Waliamuriwa kusali mara ya mwisho kwani siku zao zilikuwa zimekwisha. Sahani na familia yake yote kila mtu kwa wakati wake alisali. Utesaji ulipoanza kwa akina mama kwa kukatwa ziwa moja huku wakiwa hai bado. Hatimaye akina baba nao walionja joto ya jiwe kwa kukatwa sehemu za siri wakiwa hai. Kazi ya mwisho ilikuwa kuuwawa kwa familia ya Pandasahani. Maiti zao ziliachwa porini.
Baada ya kubainika mauaji haya, polisi walikuja, lakini mzee Mwanamabonde alikana akasema hajui kwani halikuwa eneo lake. Polisi wakamwacha huru.

Mzee Mwanamabonde akazuru Kahama kueneza mbinu za kuanzisha Sungunsungu. Akiwa wilayani Kahama, alikutana na mzee Kishosha, mzee Jugi na wengine walioonekana wazuri na maarufu. Aliwaelezea azma yake ya kuanzisha sungusungu. Aliwapa mbinu aliyokuwa akitumia huko kwake.

Harakati hizi za kuanzisha sungusungu zilizagaa na kutafsiriwa kuwa wanaanzisha chama cha siasa. Mkuu wa wilaya Kahama alimwarifu Rais kuwa kuna chama cha siasa kimeanzishwa Kahama. Rais aliagiza mara moja watu hao wafunguliwe na mashitaka. Kweli muda mrefu haukupita watu hawa akina mzee Jugi, mzee Kishosha na wengine wakahukumiwa kifungo cha miezi kumi kila mmoja.

Tume iliteuliwa baadaye walifanyia uchunguzi chama hiki. Katika Tume hiyo akiwemo Mbunge wa Maswa Mheshimiwa Shillingi na wengine. Katika kuwahoji wazee hao waliokuwa wakituhumiwa, Mheshimiwa Shillingi aliwataka waongee kisukuma. Wazee hawa kila mmoja alidai wamechoshwa na wezi. Hapakujitokeza suala la kisiasa hata kidogo.

Tume ikawasilisha taarifa yake kwa Mheshimiwa Rais, muda si mrefu Rais akamuru watu hao waachiliwe mara moja na waendelee kuunda sungusungu yao kwa minajili ya ulinzi wa ng’ombe wao na mali zao nyingine. Katika eneo la Lubaga sungusungu wamefanikiwa kwa kiasi kikiubwa katika utendaji wao wa kazi za kila siku na kusaidia watu kuishi katika amani na usalama.chombo bila nahodha huenda mrama ndivyo inavyokuwa sungusungu wa Lubaga wao kama wao wana utawala wao.
Hakika jeshi la jadi halikuwa na mzaha hata kidogo kwani katika utawala wake kulikuwa na Mtemi (Ntemi) ambaye alichaguliwa kwa kigezo cha kuwa na maarifa ya tiba za jadi au za asili ,na huacha madaraka kwa muda wa miaka mitatu labda aumwe,afe,ahame ndio amejivua uongozi na uongozi haufuati ukoo fulani bali huchaguliwa na wananchi wenyewe.msaidizi wake aliyeitwa Mwambilija “Mtwale”,katibu wake aliitwa mwandiki na msaidizi wake pia kuna kamamanda mkuu aliyetwa kwa jina la asili la Nsumba ntale na wajumbe wa kamati.Katika uongozi wao hawana kiongozi mwanamke kwa minajili ya kwamba wanawake hawawezi kutunza siri lakini kwa uchunguzi tulioufanya kuna matawi mengine kuna wenyeviti wanawake mfano mzuri ni katika kijiji cha Mwagala.
Katika jamii ya wasukuma kuna kuwa na penga mbili (filimbi)viongozi wa familia wanakuwa nazo yaani mama na baba popote wakitokewa na tatizo wanapiga sungusungu na watu wengine wanakuja na katibu anaandika tatizo lililotokea .
“Ndulilu”ni kipande cha kibuyu kilichotobolewa katika sehemu tatu na sehemu mbili zinazibwa sehemu moja inatumika kwa kupiga endapo tu kuna tatizo kubwa mfano wizi wa mifugo na mauwaji.
Tukumbuke kuwa ulinzi wa jadi ni sheria ndogondogo tuliojiwekea ili kujilinda na mali zetu .Endapo mtu ameenda kinyume na sheria tuliojiwekea hupewa adhabu maarufu kama kupigwa “mchenya”ambazo ni faini ndogo ndogo na ukiendelea wanakutenga (kumtulija)ina maana usishiriki katika shughuli zote za jamii ukifiwa watu wanakuja kuzika lakini sungusungu wanawafukuza ndugu zako kuwafariji na kulala matangani na ukifa utakuwa umeikomboa jamii yako.Ukiwa mjeuri,mwizi,unaharibu mazingira kwa kiasi kikubwa unapelekwa kujikomboa katika jeshi jingine na unatozwa faini kubwa Na adhabu zao haziangalii jinsi wala umri.
Kila kwenye mafanikio hakukosi kuwa na matatizo ndivyo ilivyo kwa wenzetu hawa sungusungu hawana vifaa vya ulinzi vya kisasa ,isitoshe kuna watu ambao hukutwa nyakati za usiku lakini si wezi na kwa upande wao yaani sungusungu wenyewe wanakuwa wanakiuka miiko yao kwa kuwa wanafiki na wenye majungu hivyo kukwamisha zoezi zima la ulinzi .
Licha ya hayo kuna mafanikio ambayo wameyapata ni kupungua kwa wimbi la wizi wa mifugo kwani vijana ndio hasa wenye ari na wito wa kulinda nchi yao na mali zao.
Sungusungu wanautaratibu wa usambazaji wa taarifa kwenda tawi jingine ujulikanao kama mwano ni taarifa ya hatari kutoka tawi moja kwenda jingine endapo kuna tatizo limetokea ili waweze kusaidiana kulitatua .Endapo mifugo imepatikana katika tawi jirani huwaarifu na kwenda kuchukua ,au wezi wamepatikana n.k.
Ikiwa mali imepatikana Mwenyewe asipopatikana kwa upande wa mifugo inatunzwa na kutangazwa kwenye matawi ya jirani baada ya miezi sita inakuwa ni mali ya sungusungu na fedha inayopatikana kutokana na faini au mifugo iliyookotwa hupelekwa katika ujenzi wa maendeleo kama vile shule na hospitali.
Kwa hali ilivyo sasa hivi kila mti una mwenyewe ukikutwa umekata mti unapelekwa kwa sungusungu na sungusungu wanakuhukumu.
Kwa upande wangu naona sungusungu ni wazuri katika suala zima la utunzaji wa mazingira hivyo basi sisi wananchi inabidi tuwaunge mkono sungusungu na kwa upande wao basi walegeze adhabu kwa aliyetengwa angalau aweze kushiriki katika masuala ya kidini tofauti na ilivyo sasa.

Serikali kutambua fursa hii iliyopo ya ulinzi wa jadi(sungusungu) ikizingatia suala la ulinzi shirikishi ambao umeonyesha mafanikio makubwa kwa taifa hili hususani vyombo vya ulinzi kwani jamii inachukua nafasi kubwa kama chanzo cha habari.
Mafunzo kwa taasisi za namna hii ni muhimu sana ili kuongeza ufanisi zaidi kwa kuzingatia ukweli na uwazi.