Tuesday, December 30, 2008

HATUA ZA VVU KATIKA MWILI WA BINADAMU

Na.Mwantumu Jongo.
Katika mwili wa binadamu ni muhimu sana kwa kila mmoja wetu kupima damu kujua kama unaishi na Virusi vya UKIMWI(VVU) au la kuna hatua tatu tofauti za VVU.

UNA VVU UNA AFYA NZURI.
Katika hatua hii inamaanisha kuwa mfumo wako wa kinga mwilini uko imara na idadi ya CD4 zako ziko juu huhitaji kutumia dawa za kupunguza makali ya vvu (ARV)kama ni mzazi waandae watoto wako kwa kuwaeleza kuhusu VVU .Hakikisha wataangaliwa vizuri pindi utakapozidiwa na ugonjwa au utakapofariki .Tafuta msaada wa kukusaidia kukabilia
na na hali hii.

UNA VVU NA UMEZIDIWA NA UKIMWI
katika hatua hiii unagua sana mara kwa mara hupati nafuu .Inamaanisha kwamba mfumo wako wa kinga ndio dhaifu sana lazima upate matibabu kwa magonjwa yako ambayo hushambulia mwili wakati kinga imepungua huitwa magonjwa nyemelezi shauriana na muhudumu wa afya kuhusu kuanza kutumia ARV. Kwa kawaida watu hufuata matibabu wakati wakiwa wagonjwa na hawajiwezi na kama unatunza mgonjwa na anatumia ARV hakikisha unaelewa vizuri kuhusu dawa hizo zungumza na muhudu wa afya kwa maelezio zaidi .

UNA VVU NA UNAANZA KUUMWA
Katika hatua hii mfumo wako wa kinga unaanza kuwa dhaifu muombe muhudumu wa afya akupime idadi ya CD4 kwenye damu yako .Hii itakuwezesha kufahamu kuanza kutumia ARV .Magonjwa unayoyapata unapokuwa na VVU yanaweza kutibika lakini lazima uwe mwangalifu kwa sababu baadhi ni magonjwa hatari ni muhimu kwenda hospitali hospitali.

MAONI
Mgonjwa ahakikishe akishajua kama ameathirika na Virusi vya UKIMWI ahakikishe anapata ushauri nasaha na kuwahi kutumia dawa za ARV kwani kwa kufanya hivyo kutamsaidia mgonjw ahuyo kuongeza muda wake wa kuishi .
Katika mwili wa binadamu ni muhimu sana kwa kila mmoja wetu kupima damu kujua kama unaishi na Virusi vya UKIMWI(VVU) au la kuna hatua tatu tofauti za VVU.

UNA VVU UNA AFYA NZURI.
Katika hatua hii inamaanisha kuwa mfumo wako wa kinga mwilini uko imara na idadi ya CD4 zako ziko juu huhitaji kutumia dawa za kupunguza makali ya vvu (ARV)kama ni mzazi waandae watoto wako kwa kuwaeleza kuhusu VVU .Hakikisha wataangaliwa vizuri pindi utakapozidiwa na ugonjwa au utakapofariki .Tafuta msaada wa kukusaidia kukabilia
na na hali hii.

UNA VVU NA UMEZIDIWA NA UKIMWI
katika hatua hiii unagua sana mara kwa mara hupati nafuu .Inamaanisha kwamba mfumo wako wa kinga ndio dhaifu sana lazima upate matibabu kwa magonjwa yako ambayo hushambulia mwili wakati kinga imepungua huitwa magonjwa nyemelezi shauriana na muhudumu wa afya kuhusu kuanza kutumia ARV. Kwa kawaida watu hufuata matibabu wakati wakiwa wagonjwa na hawajiwezi na kama unatunza mgonjwa na anatumia ARV hakikisha unaelewa vizuri kuhusu dawa hizo zungumza na muhudu wa afya kwa maelezio zaidi .

UNA VVU NA UNAANZA KUUMWA
Katika hatua hii mfumo wako wa kinga unaanza kuwa dhaifu muombe muhudumu wa afya akupime idadi ya CD4 kwenye damu yako .Hii itakuwezesha kufahamu kuanza kutumia ARV .Magonjwa unayoyapata unapokuwa na VVU yanaweza kutibika lakini lazima uwe mwangalifu kwa sababu baadhi ni magonjwa hatari ni muhimu kwenda hospitali hospitali.

MAONI
Mgonjwa ahakikishe akishajua kama ameathirika na Virusi vya UKIMWI ahakikishe anapata ushauri nasaha na kuwahi kutumia dawa za ARV kwani kwa kufanya hivyo kutamsaidia mgonjw ahuyo kuongeza muda wake wa kuishi .

No comments: